Mze Majuto
akiwa na familia yake.
Tumuombeeni!
Lejendari wa vichekesho Bongo, Amri
Athman ‘Mzee Majuto’ yu taaban kwa takribani wiki mbili sasa kufuatia
kubanwa na ugonjwa wa ngiri huku mkewe, Mama Bilal naye akisumbuliwa na homa,
jambo ambalo staa huyo ameomba Watanzania wamuombee.
KUTOKA TANGA
Katika
mazungumzo na Mwandishi kwa njia ya simu akiwa nyumbani kwake, Tanga, Mzee
Majuto alisema kuwa, ni wiki ya pili sasa hali yake kiafya si nzuri, mara
nyingi amekuwa akitumia dawa za hospitali na zile za kienyeji lakini hakuna
unafuu wowote anaoupata.
“Nasumbuliwa
sana na ngiri, sasa nakwenda wiki ya pili na siku kadhaa, hali si nzuri kabisa
na kuna kipindi nililazwa, lakini sikupata nafuu, dawa nimemeza hadi nahisi
nina stoo ya madawa tumboni, mama Bilal (mkewe) ambaye ndiye msaidizi na
mhudumu wangu, naye anasumbuliwa na homa kali, namlilia Mungu juu ya jambo
hili,” alisema Mzee Majuto.
NGIRI NI
UGONJWA GANI?
Katika
kujiridhisha kwa undani zaidi juu ya ugonjwa huo, Baadhi ya madaktari bingwa ambao
kwa nyakati tofauti walitoa ufafanuzi toshelezi juu ya tatizo hilo linalosumbua
watu wengi.
“Ngiri au
hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu
mwilini zinazoshikilia au kubeba viungo (organs) fulani kupoteza uimara au kuwa
na uwazi (opening) hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiliwa ipasavyo,”
alisema mmoja wa madaktari walioulizwa na Na Mwandishi wa Habari hii na
kuongeza:
“Tatizo la
ngiri huweza kumpata mtu yeyote. Miongoni mwa vitu vinavyoweza kumsababisha mtu
apate ugonjwa wa ngiri ni kuwa na uzito mkubwa au kuongezeka uzito kwa ghafla,
kazi ya kubeba au kunyanyua vitu vizito, tatizo la kukohoa au kupiga chafya kwa
muda mrefu, ujauzito au matatizo yanayojitokeza kwa mwanamke wakati wa
kujifungua.
Pia kuharisha au kuvimbiwa (constipation). Vitu hivyo humfanya mtu
apate ngiri (hernia).
|
No comments:
Post a Comment