Treni hiyo
pia ina mtandao kupitia WI-Fi, michezo ya kompyuta na pia mtu anaweza
kusikiliza matangazo na muziki.
|
Treni ya
Tejas Express imeanza kazi na husafiri kati ya Mumbai na jimbo la kitalii la Goa
na Treni hiyo husafiri kwa saa nane na nusu kufika Goa kutoka
Mumbai, hii ikiwa na kasi zaidi kidogo ikilinganishwana na treni nyingine.
|
Treni hiyo
ina milango ya kufunguka wenyewe, otomatiki ni ya kwanza nchini India. Inaweza
kwenda kwa mwendo kasi wa kilomita 200 kwa saa, lakini kuna udhibiti wa kasi wa
treni nchini.
Inatarajiwa
kuhudumu mara tano kwa wiki, kando na wakati wa msimu wa upepo mkali ambako
itakuwa ikihudumu mara tatu kwa wiki.
|
Tiketi za
kawaida huuzwa $18; huku za kiwango cha juu ni rupi 2,590.
Iwapo treni
hiyo itapata umaarufu maafisa wanapanga kupanua huduma wakianza na jimbo jirani
la Gujarat , kwa mujibu wa taarifa.
|
No comments:
Post a Comment