Haji Manara.
Aliyekuwa msemaji wa klabu ya Simba SC, Haji Manara
ameendelea kusisitiza kuwa klabu hiyo ndio mabingwa wa ligi kuu soka Tanzania
bara kwa msimu huu kinachosubiriwa sasa ni maamuzi kutoka FIFA kwani ubingwa
wao ni wa jasho na damu.
Kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii Manara ameandika,
‘Simba ni Bingwa wa kombe la Shirikisho, ni Bingwa wa ligi kuu ya Vodacom msimu
huu 2016/2017, ndio ni Bingwa wa nchi msimu huu, ni kusubiri tu wenye mpira wao FIFA
waturudishie points zetu tatu zilizo wazi kwa kanuni zote ili tutawazwe rasmi
kuwa machampioni wa nchi hii.
Yes no way, mchezaji awe na kadi tatu za njano zilizothibitishwa
pasina shaka yoyote na ripoti za waamuzi na makamisaa wa michezo husika na bodi
ya ligi yenye jukumu halali la kikatiba la uendeshaji na usimamizi wa ligi,
kisha eti kwa matakwa ya ajabu ya Shirikisho na kamati yake isiyo na nguvu ya
kisheria na kikanuni iipoke points Simba kwa sababu zozote zile, ni kuibaka
kanuni ambayo ipo wazi na ni dhulma isiyohitaji touchi kuiona.
INSHAALAH bingwa halali atatangazwa hivi karibuni.Yes ni
ubingwa wa Jasho na damu, ni ubingwa uliotafutwa kwa nguvu zote halali na uliomwaga
damu za wanasimba walioumia na kupoteza maisha yao katika kuusaka.
|
No comments:
Post a Comment