Kamishna
Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi Mkoani humo Benedict Wakuyamba alisema, maporomoko hayo yalisababishwa na
mvua kubwa zinazoendelea kunyesha Mkoani humo na maeneo mbalimbali nchini
"Hali
ya mvua imeendelea kunyesha na kufukia barabara eneo la Mombo kutokea Dar es
salaam kuelekea Arusha ambapo matope na miti vimesombwa na kukwama barabarani
hali iliyokwamisha magari makubwa kwa madogo kusafiri kupitia eneo hilo.
|
"Niwaombe
abiria au wananchi kwa ujumla kama hawana ulazima wa kusafiri kwenda mikoa ya
Kaskazini ni vizuri wakatulia kwa siku mbili tuone hali inakwendaje kwa ajili
ya usalama wao". Alisema Kamishna Msaidizi Benedict
Kwa upande
mwingine Kamishna huyo alisema TANROADS na Jeshi la Polisi mkoani humo
wanaendelea kusaidia kuondoa magogo na tope zilizosakama katika barabara ili
kunusuru hali ya usafiri.
|
No comments:
Post a Comment