Basi la shule ya Lucky
Vincent likiwa korongoni.
|
Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.
Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amepokea kwa mshtuko
na masikitiko mkubwa taarifa ya vifo vya wanafunzi 32 wa darasa la saba, walimu
2 na dereva wa gari la shule ya msingi iitwayo Lucky Vicent ya Arusha
vilivyotokea leo,May 06,2017 saa 3 asubuhi baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupata
ajali katika eneo la Rhotia Marera, Wilaya ya Karatu Mkoani Arusha.
Wanafunzi na
walimu hao walikuwa wakitoka shuleni kwao kwenda shule ya msingi iitwayo
Tumaini kwa ajili ya kufanya mtihani wa ujirani mwema na walipofika katika eneo
la Rhotia Marera basi walilopanda liliacha njia na kisha kutumbukia korongoni
ambako limesababisha vifo hivyo na majeruhi watatu.
Kufuatia
ajali hiyo, Rais Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Arusha
Bw. Mrisho Gambo na kueleza kuwa ajali hiyo imezima ndoto za watoto waliokuwa
wakijiandaa kulitumikia Taifa na imesababisha uchungu, huzuni na masikitiko
makubwa kwa familia za marehemu na taifa kwa ujumla.
"Ndugu
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Bw. Mrisho Gambo naomba unifikishie pole nyingi kwa
wazazi, ndugu, jamaa na marafiki wote wa wanafunzi, walimu na dereva
waliopoteza maisha, hiki ni kipindi kigumu kwetu sote, na uwaambie naungana nao
katika majonzi na maombi.
"Muhimu
kwa sasa tuwaombee marehemu wote wapumzishwe mahali pema, majeruhi wapone
haraka na wote walioguswa na msiba huu wawe na moyo wa subira, ustahimilivu na
uvumilivu katika kipindi hiki kigumu" Amesema Rais Magufuli.
Hapa chini
Taarifa kamili ya Ikulu.
|
No comments:
Post a Comment