Makamu wa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,Bi Samia Suluhu Hassan ni miongoni mwa
viongozi wakuu serikali waliohudhuria ibada hiyo.
Katika
hotuba yake kwa wananchi waliojitokeza kwa wingi katika tukio la kuaga miili
hiyo kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dakta John Pombe
Magufuli, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amewahakikishia waombolezaji
kuwa Serikali ipo pamoja nao katika kipindi hiki kigumu na chenye majonzi
mazito kwa kuondokewa na wapendwa wao.
Amehimiza wananchi kote nchini kuungana katika msiba uliotokea kwa kuwafiriji wafiwa katika kipindi hiki kigumu na kuwaombea kwa Mwenyezi Mungu azilaze roho za marehemu wote mahali peponi. |
Majeneza yakiwa kwenye meza maalum .
Makamu wa
Rais pia ameiagiza Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia, Jeshi la Polisi
nchini,walimu, wazazi na walezi wawe makini katika kuhakikisha kuwa sheria za
usalama barabarani zinazingatiwa kwa kuchukua hatua stahiki za kulinda watoto
hasa wanapotumia vyombo vya moto kwenye shughuli zao za kimasomo.
Amesema hatua hiyo itasaidia kwa kiasi kikubwa kuepusha matukio ya ajali ambayo yanaweza kuzuilika kote nchini. Makamu wa Rais amewataka madereva nchini kuzingatia sheria za usalama barabarani na waache kutumia pombe na dawa za kulevya ili kuepukana na ajali ambazo zinagharimu maisha ya wananchi. Makamu wa Rais pia amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Kenya Uhuru Kenyatta na Wakenya kwa ujumla kwa kuungana na Wananchi wa Tanzania katika msiba uliotokea.
Rais
Magufuli kupitia ujumbe kwenye Twitter, ameelezea, jinsi alivyopatwa na huzuni
kutokana na ajali hiyo.
"Nimepatwa
na uchungu na majonzi makubwa ninapoyaona majeneza ya watoto na walezi wao
waliopoteza maisha katika ajali ya basi huko Arusha. Tumewapoteza mashujaa wetu
katika elimu," amesema.
|
Majeneza yakitolewa kwenye lori na
wanajeshi wa JWTZ.
Waziri wa
elimu wa Kenya Dkt Fred Matiang'i, mmoja wa wageni kutoka nje ya Tanzania
waliohudhuria ibada hiyo, amewapa pole Watanzania kwa msiba huo.
"Kenya
itaendelea kuwa pamoja nanyi kwenye kipindi hiki kizito cha msiba huu mzito
uliowafika. Msiba huu si wa Tanzania peke yake ni wa wote hata kwetu Kenya Rais
Kenyatta na mkewe wanawapa pole sana na kuwaombea," amesema.
|
Baadhi ya waliohudhuria ibada hiyo
wamezidiwa na huzuni .
Wanafunzi
hao wa darasa la saba walifariki dunia pamoja na walimu 2 na dereva wa gari la
shule hiyo ya msingi ya Arusha baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupata
ajali katika eneo Rhotia Marera, Wilaya ya Karatu Mkoani Arusha.
Wanafunzi na
walimu hao walikuwa wakitoka shuleni kwao kwenda shule ya msingi iitwayo
Tumaini kwa ajili ya kufanya mtihani wa ujirani mwema na walipofika katika eneo
la Rhotia Marera basi walilopanda liliacha njia na kisha kutumbukia korongoni.
Wanafunzi
watatu walijeruhiwa.
Rais Magufuli,
akituma salamu za rambirambi Jumamosi alisema „ajali hiyo imezima ndoto za
watoto waliokuwa wakijiandaa kulitumikia taifa na imesababisha uchungu, huzuni
na masikitiko makubwa kwa familia za marehemu na Taifa kwa ujumla."
"Muhimu
kwa sasa tuwaombee marehemu wote wapumzishwe mahali pema, majeruhi wapone
haraka na wote walioguswa na msiba huu wawe na moyo wa subira, ustahimilivu na
uvumilivu katika kipindi hiki kigumu."
|
No comments:
Post a Comment