Mbunge wa
Geita (CCM), Mhe.Joseph Kasheku Musukuma
amesema hawezi kumsifia hata kidogo Prof.
Jumanne Maghembe, Waziri wa Maliasili na Utalii kwani yeye na watu wake wa
Wizara wanafanya mambo ya ajabu hasa kwa watu wa Kanda ya Ziwa.
Mhe.Musukuma anasema watu wa Wizara ya Maliasili
wamekuwa wakiuza ng’ombe za watu jamii ya wasukuma na kuzipiga mnada kwa dili
kwa lengo la kujinufaisha wenyewe, hivyo Mbunge huyo amesema wasukuma wameamua
kuwa wataziroga ng’ombe zote ili wanaokula ngo’mbe hizo Dar es Salaam wavimbe
matumbo.
“Napata shida sana kujiuliza labda sisi watu wa kanda ya ziwa
labda tulikuja kwa bahati mbaya Tanzania hii, mbona yanayofanyika Kanda ya Ziwa
hayafanyiki Kanda ya Kaskazini wakati nao wana mapori, Waziri ametoa siku tatu
tukamatiwe ng’ombe kwa kisingizio kwamba ni ng’ombe za Wanyarwanda wakati huo
huo watumishi wake wanaowaingiza Wanyarwanda wanawaambia toeni ng’ombe, mnaenda
kukamata ng’ombe za Wasukuma halafu unazipiga mnada na mnada wenyewe unavyopigwa
ni wa dili” alisisitiza Musukuma.
Mbunge huyo
aliendelea kuelezea namna watu wa Wizara ya Maliasili wanavyofanya minada hiyo
huku wakiwaumiza wafugaji.
“Yaani ng’ombe 600 unaambiwa ulete milioni tatu halafu wanatoa
watu wao wa Ubungo sasa hapo nikupongeze kwa sababu gani? Tunajua mipango
inayoendelea kwenye wizara yako na niliwapigia kabisa watumishi wako,
wananiambia mliipenda wenyewe kwa kauli yake kama Mwenyekiti wa Chama kesho
yake akapiga ng’ombe za watu mnada yaani ng’ombe 500 zinauzwa milioni tatu”
alisema Musukuma.
Mhe.Joseph Msukuma aliendelea na msimamo wake.
“Nataka nikwambie sisi Wasukuma sasa tumeamua na
ninazungumza uelewe tutaziroga hizo ng’ombe mtavimba matumbo mnaozila huko Dar
es Salaam, haiwezekani kwanini wanunuzi watoke Dar es Salaam peke yake yaani
leo siku ya mnada watu wametoka na malori Pugu wamejuaje kama wanakuja kushinda
kwenye minada. Mnatukamatia ng’ombe hivi hii serikali imekosa sehemu ya
kukusanya hela mpaka mkanyang’anye ng’ombe za wafugaji haiwezekani Mh. Maghembe”
HAPA CHINI NIMEKUWEKEA VIDEO UMTAZAME MSUKUMA AKITOA POVU BUNGENI.
|
No comments:
Post a Comment