Hili ni
kombe la Pili kwa Kocha Mourinho anashinda na Man United katika msimu wake wa
kwanza. Man United walishinda Kombe la Ligi mwezi Februari.
Pia -Jose
Mourinho ameshinda Fainali zote 4 za Ulaya alizotinga kama Meneja akitwaa UEFA
CUP 2003 na UEFA Champions League 2004 akiwa na FC Porto, na UEFA Champions
League 2010 akiwa na Inter Milan.
Mourinho
amedumisha rekodi yake ya 100% ya ushindi dhidi ya Ajax katika Mechi zote 7
alizocheza nao.
|
Man United wamejumuika na Ajax, Bayern Munich, Chelsea na Juventus kuwa Klabu pekee zilizonyakua Makombe yote ya UEFA huko
Ulaya.
-Vikombe
hivyo ni UEFA Champions League, UEFA Cup
Winners' Cup, UEFA Cup/UEFA EUROPA League.
Jose Mourinho Ameeleza: “Ni mwisho wa Msimu mgumu.
Lakini ni Msimu mzuri mno!”
Aliongeza:
“Tulipendelea kufuzu UEFA Champions League kwa njia hii kupita ile ya kumaliza
Nafasi ya 4, 3 au 2! Tumetimiza lengo kwa kutwaa Ubingwa wa Kombe la Ulaya,
Taji muhimu. Sasa Klabu ina kila Taji Duniani!”
|
Kocha Jose Mourinho.
Mourinho alieleza: “Sasa tuna heshima ya kucheza
UEFA SUPER CUP na Bingwa Mpya wa UEFA Champions League kati ya Real Madrid au
Juventus watakaocheza fainali ya Champions League June 03,2017, kwa hiyo Msimu
huu ulikuwa mzuri mno!”
|
No comments:
Post a Comment