Waziri Nchemba na Maagizo Kwa Polisi Kuhusu Kutekwa kwa Msanii Roma. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, April 08, 2017

Waziri Nchemba na Maagizo Kwa Polisi Kuhusu Kutekwa kwa Msanii Roma.

Msanii wa hip hop Roma Mkatolikia alikamatwa April 5,2017 usiku ambapo taarifa zilianza kuenea katika mitandao ya kijamii kuwa alikamatwa studio za Tongwe Records  na watu wasiojulikana akiwa na wenzake na wakapelekwa  kusikojulikana.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi wa Tanzania, Mhe.Mwigulu Nchemba ambaye ndio anahusika na usalama wa raia, ametumia ukurasa wake wa instagram kuonesha kuguswa na tukio la kutekwa kwa Roma Mkatoliki na Moni.

Waziri Nchemba ameeleza kuwa amewaagiza polisi kufuatilia na kutoa taarifa kwa umma.

Nimeshtushwa kwa kutokuonekana kwa Msanii Roma na Wenzake mpaka sasa. Nimeshtuka zaidi nilipofuatilia na kuambiwa hakuna kituo chochote cha polisi kinachowashikilia. Nimeelekeza Polisi wafuatilie kwa karibu kujua undani wa tukio hili na hatima yao na kutoa taarifa kwa umma
Soma hapa zaidi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad