Mkutano
na wanahabari ukiendelea.
Akizungumza
na wanahabari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa
Mlipakodi, Richard Kayombo, amesema kuwa katika mwezi Machi 2017
mamlaka hiyo imekusanya jumla ya Sh. Trilioni 1.34 ukilinganisha na Trilioni
1.31 ya mwezi Machi mwaka 2016 ambapo ni sawa na ukuaji wa asilimia 2.23.
Aidha
alisema kuwa TRA inawashukuru walipa kodi wote ambao wameitikia wito wa kulipa
kodi ya serikali kwa hiari kila wakati na hivyo kuiwezesha kutimiza wajibu wake
wa kisheria.
“TRA inatoa
wito kwa kila mlipa kodi kuwajibika kulipa kwa wakati pamoja na kufichua wale
wasiotimiza wajibu wao kikamilifu ili serikali iweze kutimiza malengo
yaliyokusudiwa kwa wananchi wake,” alisema.
“Lengo la
mwaka la TRA ni kukusanya Trilioni 15.1 ambazo tuna imani kwa kipindi
kilichobakia cha Aprili hadi Juni mwaka huu tutazifikisha kutokana na
kodi mbalimbali,” aliongeza.
Vilevile
alisema kuwa matumizi ya EFD pamoja na zoezi la uhakiki wa TIN katika mikoa ya
Arusha, Kilimanjaro, Mwanza, Dodoma, Mbeya, Morogoro, Tanga, na Pwani
linaendelea hivyo wananchi wameombwa kuhakikisha wanatumia mashine za EFD na
wale wa mikoa husika wanahakiki TIN zao ili kuepuka usumbufu unaoweza
kujitokeza.
“TRA inatoa
wito kwa mlipa kodi yeyote mwenye malalamiko, maulizo au shida yoyote kuhusiana
na masuala ya kodi kuwasiliana na ofisi ya TRA iliyo karibu naye au kupiga simu
katika kituo cha Huduma kwa Mteja namba 0800750075/0800780078 au barua pepe
huduma@tra.go.tz kwa ajili ya ufafanuzi na kutatuliwa shida yake.
Na Denis
Mtima/GPL
|
Tuesday, April 04, 2017
TRA Tanzania Yakusanya Trilioni 10.87/= Kwa Kipindi cha Miezi Tisa.
Tags
# HABARI
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
HABARI
Labels:
HABARI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment