Makamu wa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye
picha ya pamoja wachezaji wa timu ya Taifa ya Vijana (Serengeti Boys) mara
baada ya kula nao chakula cha jioni ambapo aliwaalika kwenye makazi yake Oyster
Bay, Dar es Salaam.
Timu ya
Taifa ya Tanzania ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 maarufu kama
Serengeti Boys, inatarajiwa kusafiri kesho saa 10.45 jioni kwa Ndege ya Shirika
la Ndege la Emirates kwenda Morocco kupitia Dubai, Falme za Kiarabu (UAE).
Timu hiyo
yenye Wachezaji 23 na Viongozi Wanane watakuwa Uwanja Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Mwalimu J.K. Nyerere kuanzia saa 7.00 mchana kwani wanatakiwa
kuanza kuingia uwanjani saa 7.45 kwani saa tatu baadaye ndipo ndege itakapopaa.
Wanahabari
wanaweza kupata mahojiano ya mwisho kadhalika kupata picha za habari wakati huo
wa mchana kabla hawajaingia ndani kwenye ukaguzi wa taratibu za (check in
logistics).
Kabla ya
kusafiri, timu hiyo ilikuwa kambini hapa nyumbani tangu Januari 29, mwaka huu
2017 na baada ya kambi ya mwezi mmoja na nusu, ilicheza mechi tatu za kirafiki
za kimataifa.
|
Waziri wa
Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe akizungumza wakati
wa hafla fupi ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania kwa timu ya Serengeti Boys,jana usiku tarehe 04, Aprili
2017, Oyster Bay jijini Dar es Salaam.
Machi 30,
2017 ilicheza Burundi ‘Intamba Murugamba’ na kushinda mabao 3-0 kabla ya
kurudiana tena Aprili 1, mwaka huu na kushinda mabao 2-0. Mechi zote mbili
zilifanyika Uwanja wa Kaitaba, ulioko Bukoba mkoani Kagera.
Mechi ya
mwisho hapa nyumbani ilifanyika Aprili 3, mwaka huu dhidi Ghana ‘Black
Starlets’ na kutoka sare ya 2-2 katika mchezo ulifanyika Uwanja wa Taifa, Dar
es Salaam.
Serengeti
Boys ilitumia mchezo kama ishara ya kuwaaga mamilioni ya Watanzania kabla ya
kusafiri kwenda kwenye fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana
zitakazofanyika Gabon kuanzia Mei 14, mwaka huu.
|
Waziri wa
Habari Utalii Utamaduni na Michezo Zanzibar Mhe. Rashid Ali Juma akizungumza
wakati wa hafla ya chakula cha jioni kwa timu ya Taifa ya Serengeti Boys
iliyoandaliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia
Suluhu Hassan.
Serengeti
Boys itakuwa Rabat, Morocco kufanya kambi ya takribani mwezi mmoja kuanzia
Aprili 5, mwaka huu. Ikiwa huko angalau itacheza mechi za kirafiki zisizopungua
mbili dhidi ya wenyeji morocco na timu nyingine ya jirani ama Tunisia au Misri.
Kambi hiyo
ya Morocco itamalizika Mei mosi, mwaka hu ambako timu itasafiri hadi Cameroon.
Ikiwa Cameroon, timu itacheza mechi mbili za kirafiki za kimataifa dhidi ya
wenyeji yaani Mei 3 na 6, mwaka huu kabla ya kusafiri Mei 7, mwaka huu,2017 kwenda
Gabon ambako Serengeti Boys imepangwa kundi B pamoja na timu za Mali, Niger na
Angola.
Vipimo vya
mechi dhidi ya Ghana kadhalika hapo baadaye Cameroon, vitakuwa mwafaka kwenye
kufanya tathmini ya uwezo wa Serengeti Boys kwani wapinzani hao wamekuwa na
rekodi nzuri kwenye soka la vijana na kwa kipindi hiki zimepangwa kundi A
pamoja na wenyeweji Gabon na Guinea.
|
Nahodha wa
timu ya Serengeti Boys akizungumza kwa niaba ya wachezaji wenzake mbele Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan (kulia)
wakati wa hafla fupi ya kuwatakia heri Serengeti Boys ambao wanajiandaa na
fainali ya Mataifa ya Afrika kwa vijana chini ya umri wa miaka 17
yanayotarajiwa kufanyika Nchini Gabon.
Kila la
kheri Serengeti Boys katika mapambano ya kuwania ubingwa wa Afrika kadhalika
kucheza fainali za Kombe la Dunia hapo Novemba, mwaka huu,2017 zitakazofanyika
India.
Serengeti Boys inaweza na Mtanzania tunakuomba kuichangia timu hii kwa
namna ya 223344 kupitia mitandao yote ya simu.
|
No comments:
Post a Comment