Haji Manara.
Rais wa
klabu ya Simba baada ya kushauriana na kamati ya utendaji ya klabu,imeamua
kusitisha maandamano iliyopanga kuyafanya Jumanne ijayo, baada ya nia na
dhamira njema ya serikali kutaka kushughulikia sintofahamu inayoendelea baina
ya klabu na Shirikisho la Soka nchi (TFF).
Ikumbukwe
jana klabu yetu kupitia kwenye barua iliosainiwa na Rais wetu Evans Aveva,
iliandika kwa Jeshi la Polisi nchini ikiomba kibali cha maandamano ya amani,
yaliyopangwa kuhudhuriwa na viongozi,wanachama na washabiki wa klabu, kwenda
Wizara inayosimamia Michezo nchini, ili kupeleleka kilio chetu juu ya TFF.
Kwa namna
inavyoshughulikia malalamiko ya muda mrefu na ya sasa ya klabu hii kubwa
nchini.
Katika barua
ilioandikwa na katibu Mkuu wa Baraza la michezo nchini (BMT), Kwa niaba ya
Serikali,imetutaka Shirikisho na Klabu kutafuta namna sahihi na iliyo na weledi
katika kushughulikia changamoto hizi zinazoweza kuvuruga amani ya nchi.
Serikali
kupitia barua hiyo,imeahidi pia kutukutanisha pande zote haraka
iwezekanavyo,ili kwa pamoja tumalize sintofahamu hii. Klabu ya Simba haina
mashaka yoyote na Serikali na vyombo vyake, hivyo inaamini itaitisha kwa
uharaka mkutano huo muhimu kwa maslahi ya pande zote mbili na mchezo wa Soka
kwa ujumla.
Tunawaomba
wanachama na washabiki wetu watulie na sote tuache majibizano yoyote ili kutoa
fursa kwa Serikali kusimamia kikamilifu jambo hili na kwa sasa tunafanya
taratibu na Jeshi la Polisi nchini kuwajulisha kusudio letu la kusitisha
maandamano hayo.
IMETOLEWA
NA
Haji S Manara
Mkuu wa
Habari wa Simba SC.
|
No comments:
Post a Comment