Akirusha
ndege isiyotumia Rubani katika kituo Kiteule cha Nyakanazi Bw. Parmena Pallangyo Afisa Wanyamapori kutoka
Pori la Akiba la Lwikwika Lumesule lililopo Wilayani Masasi Mkoani Mtwara alisema
ndege hizo zina uwezo wa kusafiri zaidi ya Kilometa 10 kwa muda mfupi zikiwa
zinapiga picha mnato na picha za video kwa kuonesha viwianishi (coordinates) za kila eneo kila kitu kilichopo ardhini.
“Badala ya
kuangaingaka na kutumia rasilimali magari, mafuta au rasilimali watu kwenda
kutafuta mifugo katika maeneo ambayo hatuna uhakika, tunazituma kwanza ndege
hizi zinatuletea taarifa za picha na eneo walipo mifugo pia picha hizo zinakuwa
na viwianishi (coordinates) ambazo
zinatusaidia kujua eneo husika ndipo sasa vikosi vinaelekezwa eneo husika na kwa
kutumia kifaa kiitwacho GPS huwawezesha kukamata mifugo hiyo.” Alifafanua Bw. Parmena
|
Wafugaji na Wafanyabiashara wa
Ng’ombe wasemaje?
Katika Mnada
wa Ng’ombe wa Rusahunga ambao hufanyika kila siku ya Alhamisi kila wiki
wanunuzi wa Ng’ombe wanasema kuwa kwasasa Ng’ombe wanapatikana kwa wingi katika
Mnada.
Bw. Sena Elias Magoma mnunuzi
alisema kuwa kwa Ng’ombe aliyekuwa anauzwa bei ya shilingi 1,200,000/= wiki mbili zilizopita kwasasa anauzwa bei ya
shilingi 800,000/= hadi 700,000/= na aliyekuwa anauzwa shilingi 500,000/=
kwasasa anauzwa shilingi 300,000/= hadi 250,000/=.
Naye Bw.
Fikiri Matenya Mashine ambaye ni mfugaji
alisema kuwa katika mnada huo kwa sasa Ng’ombe ni wengi kiasi kwamba bei
imeshuka sana na wafugaji wanawarudisha ng’ombe wao nyumbani kwakukosa soko.
Akiulizwa sababu ya ngo’ombe kuwa wengi katika mnada huo wa Rusahunga kwasasa
na bei kushuka alisema;
|
“Mimi
nadhani kutokana na ‘parancha’ (akimaanisha operesheni) linaloendelea huko maporini
ndiyo maana ng’ ombe wamekuwa wengi katika mnada na pengine matajiri wanasubiri
mnada wa ng’ombe ambao Serikali imewakamata ili wawanunue kwenye mnada kwa bei
ya chini sana.
Lakini mimi naona Serikali imefanya jambo jema hawa Wafugaji
kutoka nje ya nchi wanatunyanyasa sana kama watondoka mimi naamini kuwa malisho
yatatutosha sisi wenyeji.” Alifafanua Bw. Mashine
Aidha, Afisa
Mifugo anayesimamia Mnada wa Rusahunga Bw. Raphael Barakekenwa alisema kwa
kipindi hiki cha operesheni mifugo hasa ng’ombe wamekuwa wengi mno kiasi kwamba
wanakosa soko lakini Serikali kuu na Halmashauri zinapata mapato ya kutosha
kutokana na wingi wa ng’ombe mnadani.
Pia alitoa angalizo kuwa kwa wiki mbili
au tatu zijazo huenda kukawa na uhaba mkubwa wa nyama sokoni kwasababu ng’ombe
wengi kuondolewa maporini na kusafishwa kwenda mikoani na nje ya nchi.
Vilevile
katika mnada huo Mwandishi wa habari hii alishuhudia malori mengi yakiwa
yanapakia ng’ombe kwa wingi na kuondoka kuelekea mikoani pia ng’ombe wengi
wakiwa katika eneo hilo la mnada wa Rusahunga wakisubiri kununuliwa aidha
wafugaji wengine wakiamua kurudi nyumbani na ng’ombe wao waliokosa soko katika
mnada huo.
|
No comments:
Post a Comment