Taswira Picha ya Mafuliko leo April 8, 2017 Mjini Bukoba-Kagera. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, April 08, 2017

Taswira Picha ya Mafuliko leo April 8, 2017 Mjini Bukoba-Kagera.

Zaidi ya Kaya 100 zimeathirika na mafuriko yaliyosababishwa na mvua iliyonyesha usiku wa kuamkia leo April 8, 2017 .

Mkuu wa wilaya Bukoba,mkoani Kagera,Bw. Deodatus Kinawilo  akiongea na waaandishi wa habari eneo ya Nyakanyasi yalipotokea mafuriko wakati wakiendelea na zoezi la uokoaji amesema kuwa Watu Zaidi ya 70 wameokolewa kufuatia kukumbwa na mafuriko hayo lakini pia wapo waliookolewa na wananchi kwa kutumia kamba ambao idadi yao haikujulikana.



Alisema serikali imelazimika kutumia mitumbwi kufanya shughuli za uakoaji katika maeneo ya kandokando ya mto Kanoni yaliyoathirika Zaidi kwa kutumia kikosi cha zima moto ( fire ) Bukoba.

Mpaka sasa Tathimini inaendelea kufanywa Zaidi ili kujua athari ya mafuriko hayo.







No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad