Waziri wa
habari , Utamaduni Sanaa na Michezo Dk. Harisson Mwakyembe akimsikiliza kulia
Msanii wa bongo Fleva kutoka Tanzania Ibrahim Musa aka Roma Mkatoliki
akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo
jioni hii wakati akizungumzia sakata la kutekwa kwake paoja na wasanii wenzake
katika studio ya Tongwe iliyopo Masaki jijini Dar es salaam, Roma ameiomba
serikali kuwahakikishia ulinzi wasanii pamoja na watanzania kwa ujula kwakuwa
inaoyesha hawana usalama kabisa kutokana na tukio lenyewe lilivyowatokea ,
kushoto ni Mkewa wa Msanii huyo Bi Nancy.
PICHA NA
MICHUZI JR
|
Tumekuandikia
kile alichosimulia.
Wakati
naendelea na shughuli zangu, walifika watu ambao sikuweza kuwafahamu mbaya
zaidi walikuwa na silaha za moto na amri yao ya kwanza ilikuwa ni ingia ndani
ya gari.
Baada ya kuingia tu ndani ya gari, nakumbuka wale watu walitufunga
usoni na vitambaa na kutuamuru tuiname chini kwa order ya kwamba inama chini na
usiinuke na wakiwa wameshika silaha za moto.
Hofu yetu ikatufanya wote tuiname
chini na gari ikaanza kuondoka maeneo ya studio na ikaelekea ambako sisi
hatukupajua.
Tulipofika
hiyo sehemu ambayo hatuijui tukiwa tumefungwa usoni, na walitufunga na pingu.
Tukaenda sehemu ambayo hatuijui, kwa kuhisi tu hujui chochote na ndio sehemu
ambayo tulikaa kwa siku zote tatu kwasababu ilikuwa ni Jumatano, Alhamis,
tunakuja kupata sisi usalama ilikuwa ni Ijumaa usiku kuamkia Jumamosi.
Kwahiyo
siku zote watu kilichokuwa kinaendelea huko ambako tupo na hatupafahamu, kuna
mahojiano yalikuwa yanaendelea baina yetu na wale watu, mahojiano yenyewe ndio
hizo details ambazo nasema tumesharipoti katika vyombo vya dola wanaendelea na
upelelezi, wakimaliza upelelezi, wao wenyewe wataongea watatoa taarifa.
Lakini
mahojiano hayo yaliendana na vipigo ambavyo nimeonesha majereha.
Kila mtu
alipata majereha, kila mtu alipigwa, kwahiyo mahojiano yalikuwa yanaendelea na
hizo torture mpaka siku ya Ijumaa usiku sababu hatukuwa tunaweza kugundua ni
saa ngapi.
Tulitolewa hapo tulipokuwepo na kuingizwa ndani ya gari na safari
ilipoanza hapo tukiwa tumefungwa vilevile lakini safari hiyo tulifungwa na
mdomo, tukafungwa na miguu tukiwa ndani ya gari tukaenda umbali ambao
hatukuweza kujua ni wapi mpaka kufika eneo ambalo tukatupwa tukiwa katika hali
hiyo wote wanne.
Ilikuwa ni
usiku sanam hatukuweza kujua ni wapi lakini tulifikiri ni kwenye dimbwi tu la
maji tumetupwa.
Niliweza kujifungua mimi wa kwanza nikawafungua na wenzangu,
hatukujua ni maeneo gani lakini yalikuwa maeneo ya baharini, tulikuwa na
maumivu sana.
Nilivyoweza kuwafungua wenzangu tukajikuta tuko salama, tukaanza
kutembea kwa muda kiasi na baada ya muda tukakutana na kibao fulani kimeandikwa
mahaba beach tukagundua kuwa pale ni maeneo ya Ununio.
Tulitembea kwa umbali
mrefu sana mpaka tulipoweza kupata msaada baada ya hapo tukaenda kuripoti
maelezo yote katika kituo cha polisi.
ALIPOFIKA
NYUMBANI
Tulipofika
Mbezi mimi nagonga mlango, ndani hakuna mtu, nikazunguka mlango wa nyuma
nikavunja mlango wa nyumbani kwangu. Kuingia ndani familia hakuna, hilo
lilikuwa pigo jingine kwangu sababu sikujua familia yangu nayo imeenda wapi.
hiyo ikawa hofu nyingine, kwahiyo tulichokifanya nikawaambia tubadilishe nguo
nikachukua nguo nikawa wenzangu, tutokea katika zile nguo za matatizo.
Nikawaambia kama familia haipo nadhani hapa si salama, ilikuwa inaelekea
alfajiri saa kumi saa kumi na moja ikabidi tutoke tutafute bajaji tukiwa katika
mavazi salama ikawa ni nafuu kwetu.
Tulipotafuta bajaji tukaomba namba ya simu
ya bajaji kumpigia mtu. Na mtu wa kwanza kumpigia ni bosi wetu J-Murder,
hakutuamini kwamba ni sisi kwasababu ya kile alichokuwa anajua kinaendelea
uraiani.
Habari kwa
hisani ya- Bongo5.com
|
No comments:
Post a Comment