Hadi dakika
ya 80 Simba ilikuwa nyuma kwa magoli 2-0 matokeo ambayo kama yangebaki hivyo
dakika 90 zinamalizika basi Wekundu wa Msimbazi wangekuwa kwenye nafasi finyu
ya kutwaa taji la ligi kuu msimu huu.
|
Mbao FC
wamefungwa mechi zao zote (mbili) walizokutana na Simba msimu huu. Kabla ya
kuchapwa 3-2 leo April 10, 2017, walifungwa 1-0 kwenye mchezo wa raundi ya
kwanza uliochezwa October 20, 2016 kwenye uwanja wa Uhuru, Dar.
|
Magoli ya
Simba SC yamefungwa dakika za lala salama ambapo goli lao la kwanza limefungwa
dakika ya 82 na Frederick Blagnon.
Uzembe wa
golikipa wa MbaoFC, Erick Ngwegwe ambaye aliuacha mpira udunde kisha akashindwa
kuudaka kwa usahihi ulitua miguuni mwa Blagnon akafunga goli la pili dakika ya
90+1 na kufanya matokeo kuwa 2-2.
Wakati kila
mmoja akiamini mchezo utamalizika kwa sare ya Mbao 2-2 Simba SC, Mzamiru Yassin
akaifungia Simba SC goli la tatu dakika ya 90+7 kwa shuti kali baada ya beki wa
Mbao kupiga kichwa mpira ambao ulitua kwa Mzamiru kisha kiungo huyo wa Simba SC
kuachia mkwaju uliomshinda mlinda mlango wa Mbao FC.
|
Matokeo haya
yamewaweka Simba SC kileleni mwa VPL wakiwa na Pointi 58 kwa Mechi 26 wakifuata
Yanga SC wenye Pointi 56 kwa Mechi 25 huku Kagera Sugar ni wa 3 wakiwa na
Pointi 46 kwa Mechi 26 na Azam FC, ambao Jana April 10, 2017 wametoka 0-0 na
Mtibwa Sugar huko Morogoro, ni wa 4 wakiwa na Pointi 45 kwa Mechi 26.
Mbao FC inaendelea
kubaki na pointi zake 27 ikiwa katika nafasi ya 13 kwenye msimamo wa ligi,
pointi nne zaidi ya Toto Africans ambayo ipo katika timu tatu zitakazoshuka
daraja.
|
Simba SC wataendelea
kubaki jijini Mwanza wakisubiri kucheza dhidi ya Toto Africans timu ambayo
imekuwa mwiba kwa ‘mnyama’ hususan mechi inapochezwa kwenye uwanja wa CCM
Kirumba.
|
VPL 2016/2017: MBIO ZA UBINGWA – YANGA SC v SIMBA SC.
***Tarehe Haijathibitishwa
|
No comments:
Post a Comment