Katika picha
kushoto ni Kaimu katibu mkuu wa chama cha soka wilaya ya Ngara-NDFA-Jofuramu Mohamed na Mpoto Mohamed maarufu Mpotompoto ambaye ni nahodha wa Benaco
FC walijeruhiwa ambapo pamoja na kuruhusiwa kutoka hospitalini,Mpoto Mohamed amepewa rufaa ya kwenda
hospitali ya KCMC Moshi kwa matibabu Zaidi baada ya kubainika kuumia vibaya
sehemu za kifuani na mbavuni.
|
Wadau wa
familia ya soka wilayani ngara mkoani Kagera,leo wamejitokeza kuuaga mwili wa
aliyekuwa mchezaji wa Benaco FC-Nuru Athuman aliyefariki jana kwa ajali ya gari
wakati timu yake ya Benaco FC ikienda kucheza mchezo wa kirafiki na Timu ya
Rulenge Stars –mjini Rulenge.
Nuru Athuman
amefia katika hospitali ya Nyamiaga wakati Madaktari wakijaribu kuokoa maisha
yake kutokana na kuumia sehemu kubwa ya kichwa chake na mwili wake
umesafirishwa kwa ndege kwenda kwao Babati Mkoani Manyara kwa ajili ya mazishi.
|
Ajali hiyo
iliyotokea eneo la Nyamahwa ,March 05,2017 baada ya gari walilokua wakisafiria
aina ya Toyota Carrina yenye namba za
usajili T 619 CFP kupasuka tairi la mbele kushoto na kupinduka.
Katika ajali
hiyo Kaimu katibu mkuu wa chama cha soka wilaya ya Ngara-NDFA-Jofuramu Mohamed,Juma Rasi,Sospita Rasi
na Mpoto Mohamed maarufu Mpotompoto ambaye ni nahodha wa Benaco
FC walijeruhiwa ambapo pamoja na kuruhusiwa kutoka hospitalini,Mpoto Mohamed amepewa rufaa ya kwenda
hospitali ya KCMC Moshi kwa matibabu Zaidi baada ya kubainika kuumia vibaya
sehemu za kifuani na mbavuni.
|
No comments:
Post a Comment