Mkuu wa Mkoa
wa Dar es salaam, Bw.Paul Makonda
leo Machi 15, 2017 anatimiza mwaka mmoja tangu ateuliwe kuwa Mkuu wa Mkoa na
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli Machi 13,
2016 na kuapishwa Machi 15, 2016.
Soma Baadhi
ya Sentensi zake Hapa Chini.
1.Namshukuru
Rais Magufuli kwa kusikiliza kauli ya Mungu na kunikabidhi mamlaka ktk mkoa huu
wa Dar.
2.Navishukuru
sana Vyombo vya Habari kwa kuwa daraja kati ya Serikali ya Mkoa na wananchi.
Wamefanya kazi kubwa!
3.Nawashukuru
sana vijana tuliowakamata wa mwanzo(TID na wenzake), wamekuwa mfano mzuri kwa
wenzao na Mungu awasaidie
4.Mwaka
wangu wa II nikiwa kama RC wa Dar, kasi itaongezeka maana nimekomaa sasa.
Nitahakikisha jiji linarudi kwny mstari.
5.Kuna
makampuni ya barabara mawili nimeshayapiga marufuku kwa sababu ya kujenga
barabara chini ya viwango.
6.Katika
vitu nimeweka msingi mzuri ni kinondoni, kesi za ardhi zinasikilizwa mpaka
jumamosi
7.Kazi hii
nimepewa na Mungu, acha idadi ya wanaomchukia Makonda waongezeka lakini niwe na
uhakika na Mungu wangu
8.Tumeamua
kufanya vitu hadharani kwa sababu hatutaki kupokea rushwa wala fedha haramu
9.Hatuna
kisasi na mtu, ndio maana upande huo wanapigana sisi tunacheka
10.Kupitia
fedha za dawa za kulevya, watu wamejenga maghorofa yanakwenda kwa kasi sana na
wamefanya hata thamani ya viwanja ipande
11.Fedha
hizi za dawa za kulevya zinaenda kukauka DSM ili kila mtu ale kwa jasho lake
12.Tutaanza
mfumo wa kutumia kadi ili tukusanye kodi yetu na kila mtu ale kwa jasho lake,
kuna watu wanaficha fedha
13.Kipindi
hiki ni cha kazi. Nawapongeza wote wanaofanya kazi kwa bidii na kuifanya
Serikali isimame kidete
14.Changamoto
mojawapo niliyokutana nayo ni MUDA! Muda hautoshi, nahitaji hata miaka kadhaa
ili kumsikiliza kila mwananchi
15.Changamoto
nyingine ni mazoea ya Watendaji wa Serikali ktk kutoa huduma. "Njoo
kesho" imekuwa kero kwangu na kwa wananchi
16.Kuzungushwa
kwa wananchi kunapelekea changamoto katika za Serikali za Mitaa kuletwa ofisini
kwangu. Hili nalo ni tatizo!
17.Nampongeza
sana Kamishna Sirro na Awadhi (wa Usalama barabarani) kwa kusimamia ulinzi na
usalama jijini Dar
18.Milio ya
risasi ilikuwa kawaida Dar, watu waliogopa hata kwenda Mlimani City kwa hofu ya
kuporwa. Tumeyakomesha yote hayo
19.Mtu
anataka nikae kimya wakati wananchi wangu Dar wanateseka kwa matumizi ya
DawazaKulevya... Nauliza "Wewe ni NANI?"
20.Tunapambana
kupigania ndoto za vijana na matumaini ya wazazi wao. Haijalishi tumechelewa
kiasi gani lakini hatutoacha!
21.Wapiga
dili wa Bandarini jijini Dar wamekuwa wakisumbua kwa fedha zisizo halali na
kuwasumbua wafanyabiashara halali
22.Sibabaishwi
na watu wanaonichukia wakati nikitekeleza majukumu niliyopangiwa na Rais
Magufuli kama Mkuu wa Mkoa.
23.Bureau de
Change zinatumika kufichia pesa haramu. Wiki ijayo moto utawaka, lazima
tushughulikie maficho haya.
24.Sasa
foleni jijini Dar imepunguzwa kwa kiwango kikubwa na askari. Ukifurahishwa na
trafiki toa shukrani zako, tuwape moyo.
25.Mwaka huu
wa pili tutakazia sana kwenye utumishi. Nitaanzia kwenye Serikali za Mitaa
nione jinsi wanavyowasaidia wananchi.
26.Nataka
mwananchi apate majibu kamili aendapo Ofisi ya Umma. Kama hawawezi kumsaidia
waende wao ofisi ya juu sio mwananchi.
27.Wanaoishi
mabondeni jijini Dar na wana hati halali nitawapa viwanja. Watendaji waliotoa
hizo hati nitawashughulikia!
28.Najua
wengi wanaoishi mabondeni wamepangishwa na waliolipwa fidia. Huwezi kuwa na
akili timamu ukakubali kupanga bondeni
29.Hivi
karibuni nitaelekeza wapi showroom za magari zinatakiwa ziwe jijini Dar. Nataka
magari yote yauzwe eneo moja
30.Ninawashukuru
wanasheria wetu 35 wanaotoa msaada na ushauri wa kisheria bure kwa wananchi wa
jiji la Dar wasio na uwezo
31.Tumepewa
eneo kubwa la kujenga kambi kwa ajili ya wahanga wa DawazaKulevya. Hii
itatusaidia kufuatilia mienendo yao
32.Hadi sasa
tuna watu 11,854 jijini Dar waliokubali kuacha matumizi ya DawaZaKulevya kwa
hiari. Haya ni mafanikio makubwa
33.Wengine
tukiwaita Kituo cha Polisi wanatumia Colgate na Chumvi ili wasigundulike ktk
vipimo. Tuna mbinu mpya za kuwapima
34.Kuna
wanaowatumia watoto wadogo kufanya uhalifu na kabla ya hapo wanawavutisha
bangi. Tunawasaka na tutawakamata!
|
No comments:
Post a Comment