Mwenyekiti
wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na Rais Dkt John Pombe Magufuli juzi akiwa yupo
mkoani Dodoma, alipata nafasi ya kufanya kikao na wabunge wa chama hicho ambapo
alizungumza mambo mbalimbali ambayo hafurahishwi nayo kama kiongozi mkuu wa
chama.
Rais
Magufuli alikutana na wabunge hao katika Ikulu ndogo ya Chamwino Mkoani Dodoma
ambapo miongoni mwa mambo mengi aliyozungumza nao ni pamoja na kuwaambia kuwa
anafahamu baadhi ya wabunge wanampinga Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.
"Nafahamu
baadhi yenu mnampinga Waziri Mkuu na mnataka aondolewa kwa kura ya kutokuwa na
imani naye, naomba niwaambie kuwa hamtafanikiwa. Mimi namuunga mkono msaidizi
wangu huyuo kwa asilimia 100 kwa nimejionea mwenye namna anavyoweza kufanya
kazi, "alisema Rais Dkt Magufuli na kuongeza.
"Hata
mkimuondoa, nikija kuteua mwingine nitamleta huyu huyu na endapo mtamkataa basi
nitavunja bunge wote mrudi kwenye uchaguzi."
Mbali na
hilo kiongozi huyo alitoa onyo kwa wabunge wa CCM ambao wanagawa muda wao wa
kuzungumza na kuwapa wabunge wa upinzani pindi wanapokuwa kwenye vikao vya
bunge.
Kauli hii
imekuja baada ya Mbunge wa Jimbo la Bunda (CCM), Boniface Getere kumpa dakika
tano mbunge wa Serengeti (Chadema), Marwa Ryoba kutoka kwenye muda wake wa
kuchangia ambao ni dakika 10.
Katika hatua
nyingine Mwenyekiti Dkt Magufuli amewaambia kuwa anakerwa na baadhi ya wabunge
kufifisha jitihada za serikali katika kupambana na dawa za kulevya huku
akimtuhumu mbunge mmoja kutoa siri na kuzipeleka upinzani.
Kuhusu
matangazo ya bunge kutokurushwa mubashara, Mwenyekiti wa CCM aliwaambia wabunge
hao kuwa yeye ndio aliamua iwe hivyo kutokana na wabunge wengi kuwa wapiga
porojo tu.
|
No comments:
Post a Comment