Timu ya
Simba SC itamenyana na Madini FC ya Arusha katika Robo Fainali ya Kombe la
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup
(ASFC) Machi 18, mwaka huu,2017 Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha.
Kwa mujibu
wa ratiba iliyotolewa leo,March 07,2017, Mabingwa watetezi, Yanga SC iwapo
watafanikiwa kuitoa Kiluvya United ya Pwani kesho watamenyana na Tanzania
Prisons ya Mbeya Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam Machi 18,2017.
Na kama
Kiluvya United wataitoa Yanga SC basi wao
ndiyo wataialika Prisons Uwanja wa Mabatini, Mlandizi mkoani Pwani Machi 18,2017.
Washindi wa
pili wa mwaka jana, Azam FC watamenyana na Ndanda FC ya Mtwara Uwanja wa Azam
Complex, Chamazi, Dar es Salaam Machi 18, wakati Kagera Sugar watamenyana na
Mbao FC ya Mwanza Uwanja wa Kaitaba, Bukoba siku hiyo.
Wakati huo
huo: Simba SC itamenyana na Polisi Dodoma Jumamosi katika mchezo wa kirafiki
Uwanja wa Jamhuri mjinin huo.
Mchezo huo
umeandaliwa na Chama cha Soka Dodoma (DOREFA) na Simba SC itautukia kama sehemu ya
maandalizi kabla ya kumenyana na Madini FC.
|
No comments:
Post a Comment