Sehemu ya
Mradi wa Maji wa Ng’apa mkoani Lindi ambao Rais Dkt. Magufuli ametoa miezi
minne kwa mkandarasi anayejenga mradi huo ili uweze kukamilika haraka.
PICHA NA
IKULU
|
Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa
Waziri wa Maji Mhandisi Gerson Lwenge kuhakikisha kuwa Mradi wa Maji wa Ng’apa
uliopo mkoani Lindi unakamilika ndani ya miezi mine na si vinginevyo.
|
Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na
Mbunge mteule Mama Salma Kikwete mara baada ya kuwasalimia wananchi
waliokusanyika karibu na mradi wa Maji wa Ng’apa uliopo Mkoani Lindi.
|
Akiendelea
na ziara yake mkoani Lindi, Rais Dkt Magufuli leo,March 03,2017 amekagua miradi mbalimbali ya
maendeleo mkoani humo na kutoa maagizo ili kuhakikisha wananchi wananufaika na jitihada
za serikali za kuboresha maisha yao.
Rais
Magufuli amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Lindi,
Godfrey Zambi kumnyang’anya pasi ya kusafiria (passport) Mkandarasi
anayeshughulikia Mradi wa Maji wa Ngapa hadi hapo atakapokamilisha mradi huo.
Rais
Magufuli ametoa maagizo hayo alipokwenda kukagua mradi huo wa maji ambao hadi
sasa umetumia miaka 6 kujengwa lakini bado haijakamilika.
Pamoja na kuagiza
pasi ya mkandarasi ichukuliwe, Rais Magufuli amempa miezi miwili mkandarasi
huyo kuhakikisha mradi unakamili huku RC Zambi akiwa na jukumu la kuhakikisha
kuwa mkandarasi hatoki eneo hilo la mradi.
Mradi huo
unaotarajiwa kumaliza tatizo la maji mkoani Lindi umegharimu TZS bilioni 29
ambapo hadi sasa mkandarasi amelipwa bilioni 21.
Rais Magufuli amesema kuwa
kama tatizo ni fedha ndio sababu mradi haumaliziki aambiwe ili atoe fedha
serikali kuu kukamilisha wananchi waweze kupata maji.
|
Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na
wananchi wa Ng’apa mara baada ya kutembelea mradi wa Maji wa eneo hilo ambao
unasuasua kukamilika. Rais Dkt. Magufuli ametoa miezi minne kwa Mkandarasi
kampuni ya Overseas Infrastructure Alliance Private Limited ya India
kuhakikisha kuwa inakamilisha ujenzi wa mradi huo na sio kuleta visingizio.
Mradi huo wa
maji ukikamilika unatarajiwa kuzaliwa maji zaidi ya lita milioni 6 kwa siku.
Rais
Magufuli anatarajiwa kukamilisha ziara yake mkoani Lindi leo jioni ambapo
ataanza safari ya kwenda mkoani Mtwara atapofanya ziara yake Jumamosi na
Jumapili. Katika kuhitimisha ziara yake ya siku nne katika mikoa ya Pwani,
Lindi na Mtwara, Rais Magufuli atahutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa
Nangwanda Sijaona mkoani Mtwara.
|
No comments:
Post a Comment