Radi ni Nini..? - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, March 13, 2017

Radi ni Nini..?

Radi ni mwangaza na miale ya mwanga wa umeme inayotokea wakati wa ngurumo wa mvua ya radi. Radi ni matokeo ya nguvu ya umeme inayosababishwa na kutokuwepo mlingano wa chaji za umeme katika anga au kati ya mawingu kwa mawingu au kati ya mawingu na ardhi ambayo huambatana na sauti, mkondo wa umeme hewani huonekana kama mwangaza mkali. 

 Mkondo unatoa pia joto kali na joto hili husababisha kupanuka kwa hewa ghafla, upanuzi huu huleta sauti inayosikika kama ngurumo. Radi huonekana kabla ya ngurumo kwa sababu radi ina kasi ya mwanga kuliko sauti.

Radi kutoka mawinguni kwenda ardhini inaweza kuleta hasara na madhara kwa watu au vitu, watu wengi hupigwa na radi na mara nyingi wanakufa. 

Radi husababisha moto kwenye nyumba au porini, ni vigumu radi kuweza kuzuiliwa kabisa, lakini madhara yanayosababishwa na radi yanaweza kupunguzwa kwa kutumia mbinu zinazostahili. 

Radi inayolenga ardhi huelekea kuingia sehemu ya juu mahali inapopiga, vifaa au mitambo ya kikingaradi ambayo ni chuma zilizopo juu ya dari ya nyumba na kuchimbiwa ardhini kando ya nyumba huweza kusaidia, kama radi inapiga nyumba itachukua njia ya haraka ya kufika ardhini kwa hiyo itapita kwenye vyuma bila kusababisha madhara kwa nyumba yenyewe.
Radi zinapotokea unapaswa kuepuka vilele, kwani radi huwa na madhara makubwa unapokuwa kileleni, kwa mfano juu ya mti, mlingoti. 

Ukiwa ndani ya gari wakati wa radi ni salama, kwani vyuma hukusaidia kukukinga dhidi ya miale ya radi na kuelekeza ardhini. Ukiwa mahala pa wazi pasipo na kinga unaweza kuchuchumaa na huku sehemu ya mwili ikiwa imegusa ardhi na mikono yako kati kati ya miguu. 

Kamwe usiwe ndani ya maji wala kuogelea wakati wa radi kwa sababu maji ni kiungo muhimu cha kupitisha nguvu za umeme.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad