Wajumbe
2,356 wa Mkutano Mkuu Maalum wa CCM Jana March 12, 2017 wamepitisha mabadiliko
ya Katiba ya CCM kwa kauli moja chini ya Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi
(CCM) Dkt. John Pombe Magufuli.
Mabadiliko
hayo ya CCM yamelenga katika maeneo matatu makuu ikiwa ni pamoja na Katiba ya Chama
Cha Mapinduzi, Kanuni za Uchaguzi za CCM pamoja na Kanuni za Jumuiya (UWT,
UVCCM na Wazazi).
Mbali na
hilo Mwenyekiti wa CCM Dkt. John Pombe Magufuli aliweka wazi lengo kuu la
mabadiliko hayo ni pamoja na kuimarisha chama chao na kukufanya kiendelee
kutawala na kufanya vyema siku hadi siku.
“Mabadiliko
yanalenga kuboresha mfumo na muunda wa chama chetu, wa sasa una mapungufu mengi
utakuta watendaji wanafanya majukumu yanayofanana na kugongana kimaamuzi, pia
kuliibuka vyeo vilivyo na nguvu, watu walivitumia kwa maslahi yao binafsi
japokuwa kikatiba havipo”. Alisema Magufuli
Aidha
Mwenyekiti huyo alitoa onyo kali kwa mamluki yeyote atakajitokeza kuharibu
mchakato huo kwa namna moja ama nyingine na kusema adhabu kali dhidi yake
itachukuliwa.
Pia Mwenyekiti
wa CCM, Rais Dk John Magufuli amesema chama hicho hakitambembeleza mtu
kukichangia katika shughuli mbalimbali na kuwa kwa miaka yote CCM kimekuwa
kikiomba hata kwa watu ambao hawastahili.
“Matokeo
yake wamekuwa wakitumia nafasi hiyo kudhalilisha. Hakuna tena omba omba
hatutaki kumbembeleza mtu akitaka kutuchangia atuchangie,”amesema.
Amesema kuwa
chama hicho kina utajiri unaokiwezesha kujitegemea na kwamba mwanachama atakayetumia
mali za chama kwa maslahi binafsi atachukuliwa hatua kali.
|
Katibu Mkuu
wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza mambo mbalimbali mbele ya wajumbe
waliohudhuria katika Mkutano Mkuu Maalum mjini Dodoma.
Kwa upande
wake, Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndugu Abdulrahman Kinana amedai kuwa
kumekuwa na upotoshaji mkubwa ukiendelea kuwa mabadiliko hayo yanafanywa kwa
kumlenga mtu au kundi fulani la watu na kusema huo si kweli bali wanafanya
mabadiliko hayo kwa lengo la kukijenga chama.
|
Baadhi ya
Wajumbe wa mkutano mkuu Maalum wa CCM wakishangilia kwa shangwe huku wakiwa na
mabango yao yakionesha mikoa wanayoiwakilisha.
|
No comments:
Post a Comment