Kiongozi wa
chama cha Alliance for Change & Transparency –ACT Wazalendo nchini Tanzania
Mhe.Zitto Kabwe amesema Waziri wa
habari aliyefutwa kazi Bw Nape Nnauye "ni
shujaa".
Kwenye
Twitter, Mhe. Kabwe, ambaye ni Mbunge wa Kigoma-Ujiji ,amesema amewasiliana na
Bw Nnauye ambaye amemthibitishia kwamba ni kweli ameondolewa kwenye wadhifa
wake wa uwaziri.
|
Taarifa
kutoka ikulu mapema leo,March 23, 2017 ilitangaza Waziri mpya wa habari, Waziri
wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kuwa Dkt. Harrison George Mwakyembe.
Taarifa hiyo
haikusema chochote kuhusu hatima ya Mhe.Nnauye.
Dkt Mwakyembe alikuwa akihudumu kama
Waziri wa Katiba na Sheria.
Mhe. Nnauye
kwenye Twitter amewaomba watu kuwa na subira na kuahidi kwamba atazungumza na
wanahabari baadaye leo.
|
Hapa Chini
Soma Taarifa ya Ikulu.
|
No comments:
Post a Comment