Ulipaji
mahari ni tamaduni ya miaka mingi kusini wa bara Asia.
Kitabu
kimoja cha shule katika jimbo la Maharashtra nchini India, kimezua ghadhabu
baada ya kusema kuwa watu wenye sura mbaya wanastahili kulipa mahari zaidi.
Kitabu hicho
kinasema kuwa ikiwa msichana ana sura mbaya au ni mlemavu, inakuwa vigumu kwa
wasichana kama hao kuolewa na hivyo bwana harusi na familia yake huomba mahari
zaidi.
Waziri mmoja
alivyambia vyombo vya habari kuwa aya hiyo itaondolewa.
Picha za
ujumbe huo zilisambazwa pakubwa kwenye mitandao ya kijamii.
Ulipaji
mahari na tamaduni ya karne nyingi kusini mwa bara Asia, ambapo wazazi wa bibi
harusi hutoa pesa, nguo na vito vya thamania kwa familia ya bwana harusi.
Mizozo
inaweza kuibuka kuhusu no pesa ngapi zinaweza kulipwa. Wakati mwingine wakati
bwana harusi na familia yake hawalipwi, Bi harusi anaweza kudhulumiwa vibaya.
|
No comments:
Post a Comment