Baraza la
Mitihani Tanzania (NECTA) leo Januari 31, 2017 limetangaza matokeo ya Mtihani
wa Kuhitimu Elimu ya Sekondari, Kidato cha Nne kwa mwaka 2016, mtihani
ambao ulifanyika mwishoni mwa mwaka jana ambapo ufaulu umeongezeka kwa asilimia
2.44 ukilinganishwa na ule wa mwaka jana,2016.
Katika
matokeo hayo, shule za Mikoa ya Pwani na Dar es Salaam zimeonekana kung’ara
zaidi kwa kushika nafasi za juu wakati huohuo shule 6 za Dar es Salaam
zikishika nafasi 10 za mwisho katika matokeo hayo.
Shule
zilizoingia 10 bora Kitaifa.
Shule za
Dar es Salaam zilizoshika nafasi 10 za mwisho.
Kitonga Sec
School
Nyeburu Sec
School
Mbopo Sec
School
Mbondole Sec
School
Somangila
Day Sec School
Kidete Sec
School
Katibu
Mtendaji wa barza hilo, Dkt Charles Msonde amesema kati ya wanafunzi 408,372
waliofanya mtihani, jumla ya wanafunzi 277,283 wamefaulu, wakiwemo wasichana
135,859 sawa na asilimia 67.06 na wavulana 141,424 sawa na asilimia 73.26.
Kwa upande
wa watahiniwa wa shule, Dkt Msonde amesema kuwa 244,762 sawa na asilimia 70.35
ya waliofanya matihani wamefaulu ikilinganishwa na wanafunzi 240,996 sawa na
asilimia 67.91 waliofaulu mwaka 2015.
Kwa upande
wa ubora wa ufaulu, amesema watahiniwa wa shule wenye ufaulu mzuri wa Daraja la
kwanza hadi la tatu ni 96,018 sawa na asilimia 27.60
|
No comments:
Post a Comment