WAZIRI MKUU TANZANIA 2015 – 2020:- Ni Bw Majaliwa ashinda kwa asilimia 73.5. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, November 19, 2015

WAZIRI MKUU TANZANIA 2015 – 2020:- Ni Bw Majaliwa ashinda kwa asilimia 73.5.

Waziri Mkuu Mteule wa Serikali ya Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Majaliwa Kassim Majaliwa ameshinda kwa kura za ndiyo 258 sawa na asilimia 73.5 ya kura zote zilizopigwa na wabunge leo,November 19,2015 wakati kura za hapana zikiwa 91, sawa na asilimia 25.9.

 Jina hilo  lililoteuliwa na Rais Dk. Magufuli kushika nafasi hiyo ni la Mbunge wa Ruangwa, Majaliwa Kassim Majaliwa ambaye alikuwa Naibu Waziri wa TAMISEMI katika Serikali ya awamu ya Nne ya Rais Mstaafu Jakaya Kikwete.

Bw Majaliwa, 55, amekuwa mbunge wa jimbo la Ruangwa (kusini mashariki mwa Tanzania), Jimbo la Lindi kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) tangu 2010.

Bw Majaliwa, ambaye ni mwalimu kitaaluma, atamrithi Bw Mizengo Pinda ambaye alihudumu kama Waziri Mkuu chini ya Rais mstaafu Kikwete kuanzia 2008.


Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp .

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad