UEFA LEAGUE 2015/2016:-Leo November 24 na 25 ,2015 nani Kupita….Arsenal na Chelsea Vipi..??? - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, November 24, 2015

UEFA LEAGUE 2015/2016:-Leo November 24 na 25 ,2015 nani Kupita….Arsenal na Chelsea Vipi..???

Tayari Nafasi 3 kati ya 16 za Raundi ya Mtoano ya UEFA CHAMPIONZ LIGI 2015/2016,zimeshachukuliwa na Klabu 3 na bado zipo Klabu 27 kati ya 29 zilizobaki kwenye Makundi zenye nafasi za kuchukua Nafasi 13 zilizobaki.


KLABU ZILIZOFUZU KUINGIA MTOANO.

-Real Madrid

-Manchester City

-Zenit Saint Petersburg

IFUATAYO NI HALI YA KILA KUNDI KWA MECHI ZA JUMANNE NA JUMATANO.

Jumanne Novemba 24,2015.

KUNDI E.

-Barcelona (Pointi 10) v Roma (5)
 
-BATE Borisov (3) v Bayer Leverkusen (4)

Barcelona watasonga kama Washindi wa Kundi wakipata Sare na pia wanaweza kufuzu wakifungwa ikiwa Leverkusen watashindwa kushinda.

Ikiwa BATE na Leverkusen zitatoka Sare basi watupwa nje ya Timu mbili za juu ikiwa AS Roma watashinda.

Ikiwa BATE watafungwa na AS Roma kushinda, BATE watamaliza Nafasi ya 4.

KUNDI F.

-Bayern München (Pointi 9) v Olympiacos (9)

-Arsenal (3) v Dinamo Zagreb (3)

Sare kwa Bayern na Olympiacos itawatosha kutinga Raundi ya Mtoano.

Arsenal wanahitaji kushinda na kuombea Olympiacos wafungwe ili wapate nafasi ya kuifunga Olympiacos katika Mechi ya mwisho ya Kundi na wao kufuzu lakini inabidi ushindi uwe bora kuliko Olympiacos walipoifunga Arsenal 3-2 katika Mechi yao ya kwanza.

Arsenal hawawezi kuipita Bayern.

KUNDI G.

-Porto (Pointi 10) v Dynamo Kyiv (5)

-Maccabi Tel-Aviv (0) v Chelsea (7)

Porto watafuzu kwa Sare. 

Chelsea watafuzu wakishinda na Dynamo kushindwa kupata ushindi.

KUNDI H.

-Zenit (Pointi 12, Washafuzu) v Valencia (6)

-Lyon (1) v Gent (4)

Zenit wameshafuzu na watatwaa Nafasi ya Kwanza ya Kundi wakishinda.
Valencia watafuzu wakishinda huku Gent wasishinde.

Jumatano Novemba 25,2015.

KUNDI A.

-Malmö (Pointi 3) v Paris Saint-Germain (7)

-Shakhtar Donetsk (3) v Real Madrid (10, Washafuzu)

Real Madrid wameshafuzu na watashinda Kundi hili wakiwa Namba 1 ikiwa watashinda au wakitoka Sare ikiwa PSG haishindi n ahata wakifungwa wanaweza kuwa Namba 1 ikiwa PSG itafungwa.

PSG watafuzu wakishinda au kwa Sare ikiwa Shakhtar haishindi.

KUNDI B.

-CSKA Moskva (Pointi 4) v Wolfsburg (6)

-Manchester United (7) v PSV Eindhoven (6)

Man United watafuzu wakishinda.

CSKA hawatafuzu wakifungwa. 

KUNDI C.

-Astana (Pointi 3) v Benfica (9)

-Atlético Madrid (8) v Galatasaray (4)

Benfica watasonga wakishinda na pia wakitoka Sare ikiwa Atletico itaifunga Galatasaray au kwenda Sare.

Ikiwa Benfica watashinda na Atletico hawashindi, basi Benfica watatwaa Nafasi ya Kwanza.

Atlético wanahitaji Sare kufuzu.

KUNDI D.

-Juventus (Pointi 8) v Manchester City (9, Washafuzu)

-Borussia Mönchengladbach (2) v Sevilla (3)

Man City wameshafuzu na watatwaa Nafasi ya Kwanza kwa ushindi.

Juventus watafuzu wakishinda au wakipata matokeo yeyote yale ili mradi Sevilla wasishinde.

Ili kuweka hai matumaini ya kufuzu, Sevilla lazima waifunge Mönchengladbach na kungojea Mechi ya mwisho na Juventus hapo Desemba 8 washinde ili wafuzu ingawa kwenye Mechi hiyo wasipoifunga Juve basi wabahakika ya kwenda EUROPA LIGI ambako walitwaa Ubingwa wake kwa Misimu Miwili iliyopita.

UEFA CHAMPIONZ LIGI 2015/2016 - RATIBA

**Mechi zote kuanza Saa 4 Dak 45 Usiku, isipokuwa inapotajwa.

Jumanne Novemba 24,2015.

KUNDI E

2000 BATE Borislov v Bayer Leverkusen 
         
Barcelona v AS Roma  
               
KUNDI F

Arsenal v Dinamo Zagreb  
         
Bayern Munich v Olympiakos  
              
KUNDI G

FC Porto v Dynamo Kiev  
           
Maccabi Tel Aviv v Chelsea 
       
KUNDI H

2000 Zenit Saint Petersburg v Valencia  
         
Lyon v KAA Gent   
          
Jumatano Novemba 25,2015.

KUNDI A

Malmö FF v Paris St Germaine 
             
Shakhtar Donetsk v Real Madrid 
          
KUNDI B

2000 CSKA v VfL Wolfsburg 
       
Man United v PSV Eindhoven
               
KUNDI C

1800 FC Astana v Benfica 
          
Atletico Madrid v Galatasaray 
              
KUNDI D

Borussia Mönchengladbach v Sevilla 
               
Juventus v Man City  


Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad