TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI:-Agizo la Rais Magufuli kuhusu kununuliwa vitanda hospitali ya Muhimbili Latekelezwa. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, November 22, 2015

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI:-Agizo la Rais Magufuli kuhusu kununuliwa vitanda hospitali ya Muhimbili Latekelezwa.


Magari ya Bohari ya Dawa (MSD), yakishusha vifaa tiba Taasisi ya Moi kufuatia agizo la Rais Dk.John Magufuli kulitaka Bunge kutumia sh.milioni 15 kwa ajili ya kujipongeza na fedha zilizobaki kuzipeleka katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kukabiliana na uhaba wa vifaa tiba na magodoro.

Bohari ya Dawa (MSD) imeanza kupeleka Vifaa Tiba kwenye Taasisi ya Mifupa ya Muhimbili (MOI), Vifaa ambavyo vimenunuliwa na Ofisi ya Bunge kwa agizo alilotoa Rais Dk. John Magufuli. Vifaa hivyo vilianza kupelekwa juzi katika Taasisi hiyo ili kukabiliana na uhaba alioubaini Rais  Magufuli baada ya kufanya ziara ya kushitukiza katika mapema mwezi huu.

Agizo alilolitoa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli la kutaka fedha zilizochangwa na wadau mbalimbali kwa ajili ya kugharamia hafla ya Wabunge wapya zipelekwe katika hospitali ya taifa ya Muhimbili kwa ajili ya kununulia vitanda na magodoro ya Wagonjwa wanaolala chini, limetekelezwa.

Katibu mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue amesema fedha hizo zimefanikisha kupatikana vitanda 300 vya wagonjwa pamoja na magodoro yake, shuka 600, baiskeli za kubebea Wagonjwa na vifaa vingine na kwamba hivyo vyote tayari vimepelekwa katika hospitali ya taifa Muhimbili.

Balozi Sefue ameuagiza uongozi wa Hospitali hiyo kuhakikisha vitanda vyote vimefungwa Jumapili ya November 22 2015 na kisha Rais mwenyewe atakwenda Hospitalini hapo Jumatatu ya November 23 2015 viwe vyote vimefungwa tayari vinatumiwa na wagonjwa waliokosa vitanda.

Wadau mbalimbali walichangia kiasi cha shilingi milioni mia mbili ishirini na tano (225) kwa ajili ya kugharamia hafla ya Wabunge baada ya uzinduzi wa bunge la kumi na moja Dodoma lakini Rais Magufuli aliagiza fedha hizo zitumiwe kwa kiasi kidogo kisichozidi shilingi milioni 15 na nyingine zipelekwe hospitali ya Muhimbili kutatua tatizo la uhaba wa vitanda.

Gerson Msigwa


Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano IKULU,

Novemba 21, 2015.


Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp .

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad