USPIKA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA:-Yafahamu sasa Majina ya Wagombea 8 wanaowania nafasi hiyo. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, November 16, 2015

USPIKA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA:-Yafahamu sasa Majina ya Wagombea 8 wanaowania nafasi hiyo.


Chama cha Mapinduzi CCM baada ya kumtangaza Bw. Job Ndugai kuwa mgombea nafasi ya Uspika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambapo atakutana na mgombea aliyesimamishwa na Umoja wa Vyama vinavyounda UKAWA.

 Umoja huo wa vyama vinavyounda UKAWA –CUF,CHADEMA,NCCR-MAGEUZI NA NLD,wao wamemsimamisha Bw.Goodluck Ole Medeye kugombea nafasi ya Uspika na Bi. Magdalena Sakaya kwa nafasi ya Naibu spika wa Bunge akitegewa kuleta ushindani mkali kwenye kinyang'anyiro hicho dhidi ya Dr. Tulia Ackson Mwansasu wa CCM ambaye mara baada ya kujiengua nafasi ya juu ya Uspika amechukuwa fomu upande wa Naibu spika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Majina ya watu 8 wanaowania nafasi ya uspika wa jamhuri ya muungano wa Tanzania yaliyopokelewa na katibu wa bunge Dr.Thomas Kashilila ni haya hapa.
-Peter Sarungi (AFP)
-Hassan Kisabiya (N.R.A)
-Dkt Godfrey Malisa (CCK)
-Job Ndugai (CCM)
- Goodluck Ole Medeye (CHADEMA)
-Richard Lymo (T.L.P)
-Hashimu Rungwe (CHAUMA)
-Robert Kisinini (DP)

Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp .


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad