NI JAMBO SIO RAHISI AKILINI:- Kukaa Ardhini kwa zaidi ya siku 40….Hatimaye unaokolewa ukiwa Hai..Tazama Picha hapa. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, November 16, 2015

NI JAMBO SIO RAHISI AKILINI:- Kukaa Ardhini kwa zaidi ya siku 40….Hatimaye unaokolewa ukiwa Hai..Tazama Picha hapa.


Pichani ni Manusra hao wakiendelea na matibabu muhimu kutokana kukutwa wakiwa wamedhoofika kiafya,katika Hospitali ya wilaya ya Kahama,mkoani Shinyang'a na wametolewa baada ya kukaa kwenye shimo kwa siku 41 zilizopita.

MACHIMBO (1) MACHIMBO (2) MACHIMBO (3) MACHIMBO (4)


Ofisa Habari wa Wizara ya Nishati na Madini, Badra Masoud. 

Watu watano waliokuwa wakichimba madini ya Dhahabu katika mgodi wa Nyangarata uliopo Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga wamepatikana wakiwa hai baada ya kufukiwa na vifusi kwenye mashimo ya mgodi huo kwa siku 41,zilizopita.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo,November 16,2015, Ofisa Habari wa Wizara ya Nishati na Madini, Bi.Badra Masoud amesema kuwa wachimbaji hao wanaodaiwa kuwa sita, walifukiwa na vifusi mnamo Oktoba 05, mwaka huu 2015 na kuendelea kuishi kwenye mashimo hayo huku wakila magome ya miti na udongo baada ya kuishiwa chakula walichokuwa nancho, hadi jana Novemba 15,2015 walipookolewa umbali wa kilomita 10 ndani ardhini na watano kati yao kukutwa hai huku mwenzao mmoja akidaiwa kufariki dunia.

Baada ya kupatikana wakiwa hai, manusra hao walikimbizwa kwenye Hospitali ya Wilaya ya Kahama ambako wanaendelea kupata matibabu muhimu kutokana kukutwa wakiwa wamedhoofika kiafya.

Bi.Badra amewataja waliopatikana hai kuwa ni; Joseph Bulule, Chacha Wambura, Unyiwa Aindo, Msafiri Gerald na Muhangwa Amos, Wakati aliyefariki akimtaja kwa jina la Mussa Supana.


Aidha mganga mfawidhi wa hospitali ya Kahama Dr.Joseph Ngowi amethibitisha kupokea wahanga hao wakiwa hai huku mmoja wa mashuhuda aliyefanikisha watu hao kuokolewa akisimulia jinsi alivyogudua uwepo wa watu chini ya ardhi.


Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp .

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad