NAIBU SPIKA BUNGE LA TANZANIA:-Dk Tulia Ackson apitishwa na Wabunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM). - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, November 18, 2015

NAIBU SPIKA BUNGE LA TANZANIA:-Dk Tulia Ackson apitishwa na Wabunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM).

Spika wa Bunge la 11,Bw.Job Ndugai akimwapisha Mbunge wa Kuteuliwa, Dk Tulia Ackson (CCM).

Wabunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wamempitisha Dk Tulia Ackson, kugombea nafasi ya Naibu Spika wa Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Dk Tulia awali alikua akigombea nafasi ya Spika kabla ya kuingia katika mtanange wa Naibu Spika.

Aidha Naibu Mwanasheria huyo wa zamani aliteuliwa juzi na Rais Dk John Magufuli,kua Mbunge wa kuteuliwa na Rais.
Spika,Job Ndugai akivaa joho rasmi na kuingia tena Bungeni akiongozwa na maaskari wa Bunge na kisha kuapishwa na Katibu wa Bunge.

Mbunge wa Kongwa mkoani Dodoma, Job Yustino Ndugai (55) ndiye Spika mpya wa Bunge atakayeongoza Bunge la 11 lililoanza mkutano wake wa kwanza jana November 17,2015.

Ndugai, ambaye ni Mbunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), alichaguliwa kwa kishindo, akitwaa nafasi hiyo baada ya kuwashinda wagombea wengine saba kutoka vyama vya siasa kwa kupata asilimia 70 ya kura zote zilizopigwa.

Ndugai aliyekuwa Naibu Spika katika Bunge la 10, alipata kura 254 akifuatiwa na mgombea wa Chadema, Goodluck Ole Medeye aliyepata kura 109, huku kura zilizopigwa zilikuwa 365 na kura mbili ziliharibika.

Wagombea wengine sita na vyama vyao katika mabano ambao hawakupata kura ni Peter Sarungi (AFP), Hassan Almas (NRA), Dk Godfrey Malisa (CCK), Richard Lyimo (TLP), Hashim Rungwe (Chaumma) na Robert Kasinini (DP).

Kutokana na ushindi huo, Ndugai anakuwa Spika wa sita wa Bunge hilo akitanguliwa na Adam Sapi Mkwawa kuanzia 1964 hadi Novemba 19, 1973, kisha aliingia Erasto Mang’enya Novemba 20, 1973 hadi Novemba 5, 1975, kisha alirudi tena Mkwawa kuanzia Novemba 6, 1975 hadi Aprili 25, 1994.

Wengine ni Pius Msekwa Aprili 28, 1994 hadi Novemba 20, 2005, Samuel Sitta Desemba 26, 2005 hadi Novemba 2010, kisha Anne Makinda Novemba 12,2010 hadi November ,17,2015.

Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad