MWANASOKA BORA AFRICA 2015:-Wafahamu watano wanaoiwania Tuzo hiyo ya BBC. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, November 15, 2015

MWANASOKA BORA AFRICA 2015:-Wafahamu watano wanaoiwania Tuzo hiyo ya BBC.

Wakati Shirikisho la soka barani Afrika- CAF litangaze majina ya wachezaji wanaowania tuzo ya mchezaji bora Afrika, Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) na lenyewe November 14,2015, limetangaza majina matano ya wachezaji wa Afrika wanaowania tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa mwaka 2015.
Manchester-City-v-Crystal-Palace
Yaya Toure

BBC imetaja majina matano yatakayowania tuzo hiyo,huku  miongoni mwa majina hayo matatu ni kutoka  Ligi Kuu Uingereza.

Tuzo hiyo  ilianzishwa mwaka 1992 na uhusisha waandishi wa habari kuchagua kwa kupiga kura za wachezaji watakaoingia katika Kutangazwa na baada ya hapo  watu wengine hupewa fursa ya kuchagua yupi anastahili kuibuka mshindi.
Southampton-vs-Manchester-United
Sadio Mane.

Majina matano yaliotajwa kuingia katika kipengele hicho ni Pamoja na , Pierre-Emerick Aubameyang kutokea Gabon , anacheza katika klabu ya Borussia Dortmund ya Ujerumani, Andre Ayew kutokea Ghana , anakipiga katika klabu ya Swansea, Yacine Brahimi wa FC Porto , anatokea Algeria, Sadio Mane wa Senegal, anachezea klabu ya Southampton na Yaya Toure kutokea Ivory Coast ,akiichezea Manchester City.

Porto-vs-Maccabi-Tel-Aviv
Yacine Brahimi
West-ham-v-Chelsea
Andre Ayew
1899-Hoffenheim-v-Borussia-Dortmund-Bundesliga
Pierre-Emerick Aubameyang

Mshindi ataamuliwa na mashabiki wa soka Afrika ambao watapewa fursa kupiga kura hadi tarehe 30, Novemba.

Unaweza kupiga kura Mtandaoni kwa kubofya hapa au kwa kutuma ujumbe mfupi wa simu kwa nambari….+44 7786 20 20 08:

Tuma 1 kumpigia Pierre-Emerick Aubameyang

Tuma 2 kumpigia Andre Ayew

Tuma 3 kumpigia Yacine Brahimi

Tuma 4 kumpigia Sadio Mane

 Tuma 5 kumpigia Yaya Toure

Mshindi atatangazwa Siku ya Ijumaa tarehe 11 mwezi December,2015 wakati wa matangazo maalum kwenye BBC World News na BBC World Service, wakati mitandao ya BBC Sport na BBC Africaikitoa pia matangazo. Kwa sheria na masharti bofya hapa.

Rekodi ya tuzo hizo kuanzia mwaka 2000 hadi 2014.

    2000 Patrick Mboma – Cameroon na Cagliari/Parma (Italia)

    2001 Samuel Kuffuor – Ghana na Bayern Munich (Ujerumani)

    2002 El Hadji Diouf – Senegal na Lens (France)/Liverpool (Uingereza)

    2003 Jay-Jay Okocha – Nigeria na Bolton Wanderers (Uingereza)

    2004 Jay-Jay Okocha – Nigeria na Bolton Wanderers (Uingereza)

    2005 Mohamed Barakat – Egypt na Al Ahly (Misri)

    2006 Michael Essien – Ghana na Chelsea (Uingereza)

    2007 Emmanuel Adebayor – Togo na Arsenal (Uingereza)

    2008 Mohamed Aboutrika – Egypt na Al Ahly (Misri)

    2009 Didier Drogba – Ivory Coast na Chelsea (Uingereza)

    2010 Asamoah Gyan – Ghana na  Sunderland (Uingereza)

    2011 Andre Ayew – Ghana na Marseille (Ufaransa)

    2012 Christopher Katongo – Zambia na Henan Construction (China)

    2013 Yaya Toure – Ivory Coast na Manchester City (Uingereza)

    2014 Yacine Brahimi – Algeria na Porto (Ureno)

    2015 ………………..??????????


Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad