Hawa watoto
Zahra na Zarina wamezaliwa pacha walioungana tarehe 16/11/2015 mama yao Bi Tausi Hageze akiwa njiani kwenye
boda boda akitokea kijiji cha Nyarurama, Tarafa ya Rulenge Wilaya ya Ngara,Mkoani Kagera
akielekea hopitali ya misheni Rulenge.
Alipopata uchungu wa kuzidi alimuomba
bodaboda asimame akaweza kujifungua kwa shida mbele ya mumewe anaeitwa Hamdani,
hapo njiani.
Baada ya
hapo wakapelekwa hospitali ya misheni Rulenge. Mama na watoto wako salama, kama
unavyo ona katika picha wameungana kiunoni.
Msamaria amekutana na changamoto hii hapo hospitali na
kuamua kuwasaidia kuchangisha iliwapelekwe Mwanza Bugando Hospital walipo hivi
sasa.
Inaelezwa na
ma daktari hapo, wameshauri watoto wapelekwe India kwa upasuji na matibabu
zaidi.
Msamaria
anaewasaidia Bi Sabra Said Salum wa namba ya simu +255767220099 anaomba yoyote
atakae guswa na kadhia hii afikishe mchaango kwake ili aweze kuwafanyia safari
hii muhimu kuokoa maisha ya mapacha hawa.
Baba Hamdani
Sibhoro na mama Tausi Hageze wote ni wakulima wa jembe la mkono hawana uwezo
hata wa kufika Dar.
Bi Sabra kachangisha
na kuweza kuwafikisha Bugando, kuwalipia mahitaji ya hapo.
Mungu
awabariki.
Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp .
|
No comments:
Post a Comment