Timu ya
taifa ya Tanzania bara, Kilimanjaro Stars imepata ushindi wa magoli 4-0 dhidi ya
timu ya taifa ya Somalia kwenye mchezo wa kwanza kati ya timu hizo mbili kwenye
michuano ya CECAFA Challenge Cup 2015
inayoendelea Addis Ababa, nchini Ethiopia.
Magoli ya
Kili Stars yamefungwa na Elius Maguri pamoja na John Bocco ‘Adebayo’ ambao kila
mmoja amefunga magoli mawili kwenye mchezo huo.
Bocco
alianza kuifungia Kili Stars goli la kwanza dakika ya 12 kwa mkwaju wa penati,
Elius Maguli akapachika bao la pili dakika ya 17 na 54 kisha Bocco akahitimisha
ushindi wa magoli 4-0 kwa kufunga bao dakika ya 55.
Kili Stars
inayonolewa na kocha Abdallah Kibadeni ‘King Kibadeni’ ipo kundi A pamoja na
timu za Ethiopia, Somalia na Rwanda.
Kili Stars itakutana na Rwanda kwenye
mchezo wake wa pili siku ya Jumanne,November 24,2015 huku ikiwa inahitaji ushindi ili
kujihakikishia kusonga mbele moja kwa moja kwenye hatua inayofuata ya
mashindano hayo
Ikumbukwe
jana,November 21,2015 timu ya visiwani Zanzibar ‘Zanzibar Heroes’ ilipoteza mchezo wake wa
ufunguzi dhidi ya Burundi kwa bao 1-0.
Michuano hiyo imeanza rasmi November 21
na inatarajiwa kumalizika December 6 mwaka huu.
KUNDI A
|
KUNDI B
|
KUNDI C
|
Ethiopia
Rwanda
Tanzania
Somalia
|
Kenya
Uganda
Burundi
Zanzibar
|
Sudan Malawi South Sudan Djibouti
|
RATIBA/MATOKEO.
**Saa: Mechi
ya Kwanza Saa 10 na ya Pili Saa 12
Jumamosi
Novemba 21,2015.
Burundi 1 –
0 Zanzibar
Ethiopia 0 –
1 Rwanda
Jumapili
Novemba 22,2015.
Somalia 0 –
4 Tanzania
Kenya Vs
Uganda
Jumatatu Novemba 23,2015.
S. Sudan v
Djbouti
Sudan v
Malawi
Jumanne Novemba 24,2015.
Zanzibar Vs
Uganda
Rwanda Vs
Tanzania
Jumatano Novemba 25,2015.
Kenya Vs
Burundi
Somalia Vs
Ethiopia
Malawi v
Djibouti
S. Sudan v
Sudan
Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp .
|
No comments:
Post a Comment