![]() |
|
Ni katika
Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 25,2015 ambapo Kila kituo kitakuwa na watu
450 watakaotumia saa tisa huku Watu 52,000 waliojiandikisha mara mbili nao
kupiga kura......
Ikiwa
zimebaki siku 47 kabla ya kufanyika Uchaguzi Mkuu, imebainika kuwa kila mtu
atatumia wastani wa dakika moja kupiga kura kuchagua diwani, mbunge na rais.
Mwenyekiti
wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Damian Lubuva amesema kila kituo
kitakuwa na watu 450 watakaopiga kura kuanzia saa 2.00 asubuhi mpaka saa 10.00
jioni.
Hiyo ina
maana kwamba, kuanzia saa 2.00 mpaka saa 10.00 jioni ni sawa na saa tisa,
ambazo ni sawa na dakika 540. Kwa sababu kila kituo kitakuwa na watu 450, ina
maana kuwa watu hao watatakiwa kupiga kura ndani ya dakika 540 ambazo ni sawa
na dakika 1.2 kwa kila mtu.
Kwa mujibu
wa NEC, muda huo wa saa 10.00 jioni ni wa kufunga vituo, lakini watu ambao
watakuwa katika mistari mpaka wakati huo wataendelea kupiga kura mpaka
watakapomalizika.
Watu
watakaojitokeza kuanzia muda huo hawataruhusiwa kupiga kura. Kituo kimoja watu
450 Lubuva amefafanua kuwa wakati wa uandikishaji, vilitumika vituo 37, 848
lakini wakati wa upigaji kura vitaongezeka ili wote waliojiandikisha wapate
fursa ya kupiga kura kwa sababu tofauti na uandikishaji, upigaji kura ni kazi
ya siku moja tu tena kwa saa zisizozidi tisa.
Alifafanua
kuwa ongezeko la vituo hivyo linalenga kuwahudumia Watanzania wote 23,782,558
waliojiandikisha kushiriki uchaguzi wa mwaka huu, akibainisha kuwa kwa mkakati
ulioandaliwa, kila kituo kitatakiwa kuhudumia wapigakura wasiozidi 450 kwa saa
tisa za siku hiyo, zitakazotumika kuamua mustakabali wa uongozi wa Tanzania kwa
miaka mitano ijayo.ZAIDI TAARIFA HII BOFYA HAPA.
|
Monday, September 07, 2015
UCHAGUZI MKUU 2015 TANZANIA:-Kupiga kura dakika moja.
Tags
# HABARI
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
HABARI
Labels:
HABARI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.






No comments:
Post a Comment