KAMPENI ZA CCM 2015:- JK na DKT. Maguful wauteka Mji wa Morogoro . - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, September 07, 2015

KAMPENI ZA CCM 2015:- JK na DKT. Maguful wauteka Mji wa Morogoro .

Rais Kikwete na mgombea wa Urais kwa Tiketi ya CCM Dkt. John Pombe Magufuli na viongozi wengine  katika Uwanja wa Jamhuri Mjini Morogoro ,Jana September 06,2015,Jumapili wakati wa  mkutano wa kampeni wa mgombea huyo wa urais kwa tiketi ya chama hicho tawala .

Mmgombea Urais  Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk.John Magufuli amesema iwapo atachaguliwa kuwa Rais katika uchaguzi mkuu mwaka huu(October 25,2015) ,Serikali yake itashusha bei ya vifaa vya ujenzi hasa bati na saruji. 

Dk.Magufuli alitoa kauli hizo jana wakati anazungumza kwa nyakati tofauti katika maeneo ya Mkamba,Ruaha,Mikumi,Kilosa mjini pamoja na Morogoro mjini ikiwa ni sehemu ya kuomba ridhaa ya kuomba kichaguliwa urais katika uchaguzi mkuu mwaka huu.

Alisema kuwa serikali yake inataka kurahisisha maisha ya watanzania wote na hivyo atapunguza bei ya saruji na bati na hilo litafanikiwa kwa kupunguza ushuru wa vifaa hivyo."Serikali ya Magufuli nataka iwe ya kurahisisha maisha ya wananchi wake.Moja ya mambo ambayo ninedhamiria kuyafanya ni kupunguza bei ya bati na saruji.Nataka kuona watu wanajenga nyumba nzuri na za kisasa, hivyo lazima tushushe bei ya vifaa vya ujenzi,alisema Dk.Magufuli.

Kwa upande mwingine alisema atasimamia amani ya nchi kwani ndio msingi wa maendeleo ya taifa letu na kuongeza shida ya watanzania si vyama vya siasa bali ni maendeleo yao.Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

Rais Kikwete na mgombea wa Urais kwa Tiketi ya CCM Dkt. John Pombe Magufuli  katika Uwanja wa Jamhuri Mjini Morogoro Jumapili wakati wa  mkutano wa kampeni wa mgombea huyo wa urais kwa tiketi ya chama hicho tawala.
Sehemu ya gharika la wananchi  katika Uwanja wa Jamhuri Mjini Morogoro Jumapili kwa mkutano wa kampeni wa mgombea Urais kwa tiketi ya chama hicho tawala cha CCM.

Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad