KUKUIKA SHERIA:-TFDA yateketeza bidhaa bandia za Sh. bilioni 4.5. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, September 07, 2015

KUKUIKA SHERIA:-TFDA yateketeza bidhaa bandia za Sh. bilioni 4.5.

Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA).

Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) Kanda ya Ziwa, imekamata na kuziteketeza bidhaa zenye uzito wa tani 8.26 zisizokidhi vigezo vya ubora na usalama kwa chakula, dawa za binadamu na mifugo pamoja na vipodozi vikiwa na thamani ya zaidi ya Sh. bilioni 4.5 katika kipindi cha 2014/15.

Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na mamlaka hiyo, hatua hiyo ni utekelezaji wa Sheria Na.1 ya 2003 ya Chakula, Dawa na Vipodozi  kwa wasindikaji, wauzaji wa chakula, dawa, vipodozi na vifaa tiba.

“Bidhaa za dawa za binadamu na mifugo zenye uzito wa tani 1.8 zikiwa na thamani ya Sh. bilioni 1.2, zilikamatwa sokoni na kuteketezwa kutokana na viwango duni, bidhaa bandia pamoja na bidhaa nyingine kwa kutokuwa na usajili wa mamlaka,” ilifafanua taarifa hiyo.

Pia taarifa hiyo ilisema vipodozi vyenye uzito wa tani 3.6 vyenye thamani ya zaidi ya Sh. bilioni 2.3, vilikamatwa baada ya kukutwa na makosa ya kutokuwa na usajili wa mamlaka pamoja na vipodozi vingine kupigwa marufuku kutokana na kuwa na viambata vyenye sumu.

TFDA imewataka wafanyabiashara wa chakula, dawa, vipodozi na vifaa tiba, kuzingatia matakwa ya Sheria ya Chakula na Dawa kwa kuhakikisha bidhaa wanazozalisha, kununua, kuziuza, kuzitunza na kuzisambaza, zinakidhi vigezo vya ubora, usalama na ufanisi ili kumlinda mtumiaji wa bidhaa hizo.

TFDA imesema kazi ya kukamata na kuharibu bidhaa zinazokwenda kinyume na matakwa ya kisheria ni endelevu na itaendelea kuwachukulia hatua stahiki wafanyabiashara watakaokiuka taratibu na masharti husika.

CHANZO: NIPASHE 

Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad