![]() |
|
Mgombea
ubunge wa jimbo la Kahama, James Lembeli kupitia tiketi ya Chama cha Demokrasia
na Maendeleo-CHADEMA.
MGOMBEA
ubunge wa jimbo la Kahama, James Lembeli kupitia tiketi ya Chama cha Demokrasia
na Maendeleo (CHADEMA) ameishambulia serikali ya CCM na kueleza kwamba serikali
hiyo haiwezi kuwapatia wananchi maendeleo kutokana na kuwa na mfumo mbovu wa
kiutawala.
Mbali na hilo Lembeli alisema serikali ya
CCM ndiyo serikali pekee yenye mfumo kandamizi, viongozi wake ni walaghai wakubwa
na imekuwa na mfumo mchafu wa kulindana mafisadi kwa mafisadi huku wananchi wa
kawaida wakiendelea kutaabika.
Lembeli
ambaye awali alikuwa mbunge wa CCM jimbo la Kahama na baadaye kutimkia Chadema,
alitoa kauli hiyo wakati wa uzinduzi wa kampeni za Chadema zilizofanyika katika
viwanja vya Freeman Mbowe ambapo uwanja huo ulijengwa na mbunge anayemaliza
muda wake na kutetea jimbo hilo Prof Kulikoyela Kahigi.
Kiongozi
huyo ambaye alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa kampeni hizo alitonesha
vidonda vya wafugaji wa jimbo hilo kwa kueleza kwamba serikali imekalia ripoti
ya uchunguzi wa Tume iliyoundwa na bunge kwa ajili ya Operesheni tokomeza.SOMA ZAIDI KWA KUBOFYA HAPA..''
Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo
na Nyingine kwa kujiunga na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia
tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|
Sunday, September 06, 2015
KAMPENI UKAWA 2015:-Lembeli aanika yaliyofichwa Operesheni Tokomeza.
Tags
# SIASA
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
SIASA
Labels:
SIASA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.






No comments:
Post a Comment