UHALIFU KAGERA:-Taswira Picha ya Mazindiko yakikamatwa na Jeshi la Polisi Kagera yaliyokuwa yakitumiwa na Wahalifu wa kukata Mapanga na Koromeo Watu Manispaa ya Bukoba . - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, April 11, 2015

UHALIFU KAGERA:-Taswira Picha ya Mazindiko yakikamatwa na Jeshi la Polisi Kagera yaliyokuwa yakitumiwa na Wahalifu wa kukata Mapanga na Koromeo Watu Manispaa ya Bukoba .

Pichani kulia ni  ndiye mganga wa jadi ambaye anatuhumiwa kuwapa kinga Watuhumiwa wa kukata Mapanga na Koromeo ,Manispaa ya Bukoba ambaye ni mwenyeji wa kijiji cha Ibosa.




Hizi ni baadhi ya tunguli na madawa yaliyokuwa yakitumiwa na wakata koromeo kama kinga.

Baadhi ya waandishi  wa habari wakipata taarifa juu ya waliokamatwa kwa tuhuma ya kukata koromeo.

Afisa upelelezi wa mkoa wa Kagera Gilles Muroto akisikiliza kwa makini maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Mwaibambe.

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Kagera, Henry Mwaibambe akionyesha mazindiko yaliyokuwa yakitolewa na mganga wa jadi aliyekamatwa na Jeshi hilo yaliyokuwa yakitumiwa na wakata  Koromeo kama kinga.

Jeshi la polisi katika mkoa wa KAGERA limeanza kufanikisha mikakati yake yenye lengo la kusambaratisha mtandao wa watu wasiojulikana wanaojihusisha na vitendo vya kufadhili na kufanya mauaji ya kuwakata kata watu kwa MAPANGA na baadae  kuwanyonya damu ambavyo  katika kata za KITENDAGULO, KIBETA na RWAMISHENYE katika manispaa ya BUKOBA.

Katika kusambatarisha  mtandao huo jeshi hilo  limefanikiwa  kuwaua watuhumiwa WAWILI,  JOHANES JOSEPH  ambaye ni kinara wa mauaji ya kuwakata kata MAPANGA na EDWARD THEOPHIL ambao ni miongoni mwa watuhumiwa  WANNE  walioshikiliwa kwa tuhuma ya kuhusika na  kufadhili vitendo mauaji ya kuwakata kata WATU kwa mapanga kwa  ajili ya imani za KISHIRIKINA.

Akizungumza April 09,2015  na waandishi wa habari Kamanda wa jeshi la polisi mkoani KAGERA, HENRY MWAIBAMBE amesema watuhumiwa waliouwawa kwa kutumia nguvu za giza walikuwa wakijaribu kuwatoroka maofisa wa jeshi la polisi waliokuwa wakiwahoji wakati wakiwaonyesha  MAZINDIKO  wanayoyatumia katika kutekeleza mauaji, pamoja na kutoa onyo kwa wanajihusisha na vitendo hivyo pia amesema jeshi hilo kwamba linamshikilia   GAUDENSIA NDIBALEMA ambaye ni mganga wa jadi kwa tuhuma ya kuwapatia kinga wanajihusisha na vitendo vya mauaji hayo.

Kufuatia vitendo vya mauaji ya kukata watu kwa mapanga katika manispaa ya BUKOBA, zaidi ya watu KUMI wameishauwawa , vitendo hivyo vinahusishwa na imani za kishirikina ambapo inadaiwa kwamba wale wanaokatwa mapanga damu zao zinavyonywa na kupelekwa pasipojulikana.


Pata Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati  wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad