TATIZO LA AJALI TANZANIA:- hii imetokea leo April 29, 2015 mkoani Morogoro. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, April 29, 2015

TATIZO LA AJALI TANZANIA:- hii imetokea leo April 29, 2015 mkoani Morogoro.

Jinamizi la ajali  nchini limekuwa Likigonga vichwa Watanzania  hasa cha kushtua zaidi ni kwamba ajali hizi zimetokea mfululizo sana, watu wengi wamefariki, wengine wengi majeruhi huku Uzembe wa baadhi ya Madereva na  Mwendokasi umehusishwa vikitajwa kuwa chanzo cha ajali.

Leo April 29, 2015 huko Morogoro, watu 15 kujeruhiwa na wengine zaidi ya 50 wamenusurika katika ajali ya basi la Takbir lililokuwa likitokea mkoani Geita kuligonga basi la kampuni ya Abood katika eneo la Lubungo Mikese.

Majeruhi wa ajali hiyo wamesema chanzo cha ajali ni  dereva wa basi la Takbir kutokuwa makini na kuendesha gari kwa mwendokasi.. baada ya ajali hiyo dereva huyo alikimbia.

Kamanda wa Polisi Morogoro, Leonard Paulo amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.

Pata Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati  wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad