Wakizungumza
kwa niaba ya serikali ,Mkuu wa wilaya ya kilosa Bw John Henjewele amesema
serikali imewalazimu kufanya mazishi ya pamoja ya watu waliofariki kwenye
ajali hiyo ambao miili yao haijatambulika na kwamba serikali itaendelea
na zoezi la ukaguzi wa magari mkoani Morogoro ili kudhibiti ajali za
mara kwa mara zinazopoteza maisha ya watu huku wengine wakiachwa na vilema
vya maisha ambapo mkuu wa wilaya ya kilombero Bw Lephy Gembe
amewataka wananchi kuwa na uvumilivu katika msiba mkubwa
walioupata.
Kwa upande
wake Diwani wa kata ya ruaha, Rahel Nyangasa amesema wamepokea msiba huo
kwa masikitiko makubwa kwani umekuwa ni pigo kubwa kwa wakazi wa wilaya hizo
huku ndugu na waombolezaji wakisema msiba huo siwakusahaulika kwani umewastua
sana ambapo naye muinjilisti wa kanisa la kiinjili la kilutheri Issaya
Chura akiomba serikali kuendelea kukabiliana na madereva wabovu.BOFYA HAPA KUTAZAMA PICHA ZA AJALI HIYO YA BASI NA FUSO.
|
Pata Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630. |
No comments:
Post a Comment