PICHA / HABARI:-Taswira ya matukio ya mauji ya chuki za kibaguzi (ZENOPHOBIA) yanayofanywa na raia wa Afrika Kusini dhidi ya wageni na Tamko la Serikali ya Tanzania. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, April 20, 2015

PICHA / HABARI:-Taswira ya matukio ya mauji ya chuki za kibaguzi (ZENOPHOBIA) yanayofanywa na raia wa Afrika Kusini dhidi ya wageni na Tamko la Serikali ya Tanzania.

Picha juu na chini ni Baadhi ya Raia wa Africa Kusini wakiwa na silaha za jadi katika na vurugu zinazoendelea nchini Afrika Kusini kutokana na Raia wa taifa hilo kuwachukia Wageni, tatizo  lilianza mwaka 2008 na 2014 na kwamba lilichangiwa na Mfalme Goodwill Zwelithini wa Jamii ya Wazulu kuchochea fujo hizo dhidi wageni lakini Mfalme huyo leo April 20,2015  amezungumza na wananchi hao akiwaasa kuacha kuwaua wageni waliopo nchini humo.






Serikali ya Tanzania imesema hakuna mtanzania aliyeuawa katika matukio ya mauji ya  chuki za kibaguzi (ZENOPHOBIA) yanayofanywa na raia wa Afrika Kusini dhidi ya wageni na tayari imeanza mpango wa kuwarudisha nyumbani watanzania 21 kati ya 23 waliohifadhiwa katika kambi kwenye mjini DURBUN nchni humo kwa ajili ya usalama.

Akizungumza na waandishi wa habari leo April 20,2015,Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa Mhe. Bernad Membe (Pichani ) amesema  vifo vya watanzania watatu vilivyotokea nchni humo havina mahusiano na mauaji hayo ZENOPHOBIA na kusisitiza serikali ya afrika kusini imeanza kuchukua hatua na tayari watu watatu waliohusika na kifo cha rais wa msumbiji wamekamatwa.

Akizungumzia idadi ya watanzania waliohifadhiwa kwenye Kambi katika mji wa DURBUN,Mhe Membe amesema takribani watanzania 23 wamehifadhiwa katika kambi ya isipingo iliyo  na zaidi ya raia  wa kigeni elfu tatu ambao wako chini ya ulinzi wa serikali ya afrika kusini na kusisitiza serikali imeanza utaratibu wa kuwarudisha nyumbani watanzania 21 kati yao.

Akielezea msimamo wa Tanzania kufuatia mauaji hayo ya ZENOPHOBIA yanayoendelea nchni afrika kusini,Mhe. Membe amesema serikali inaunga na jumuiya ya nchi za SADC kulaani vitendo vya mauaji yanayoendelea nchni humo ambapo watu 8 wamekwisha uawa kikatili na kuita serikali ya afrika kusini kuzuia mauaji hayo haraka iwezekanavyo.

Aidha amesema serikali ya Tanzania haitakuwa na tatizo la Watanzania kurudi nchni humo baada ya mauaji kudhibitiwa na kwa upande wa wafanyabishara walisajiliwa kihalali na kupoteza mali zao, serikali itawasiliana na wanasheria wake ili kuona namna ya kutafuta namna ya nchi hiyo kuwafidia hasara waliyoipata.

Amesema tatizo hilo lilianza mwaka 2008 na 2014 na kwamba lilichangiwa na Mfalme Goodwill Zwelithini wa Jamii ya Wazulu kuchochea fujo hizo dhidi wageni lakini Mfalme huyo leo na amezungumza na wananchi hao akiwaasa kuacha kuwaua wageni waliopo nchini humo

Waziri Membe amewataja Watanzania waliofariki nchini Afrika Kusini kwa sababu ambazo ni tofauti na vurugu hizo kuwa ni Bw Rashid Jumanne aliyeuawa baada ya kufanya unyang'anyi, Athuman China aliyechomwa kisu akiwa gerezani kwa vurugu na Ally Mohamed aliyekuwa na ugonjwa wa kifua kikuu na kwamba mwili wake umeletwa nchini jana April 19, 2015.

Pata Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati  wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

1 comment:

Post Bottom Ad