MAFANIKIO YA ELIMU:-Taswira Picha Wadau wa elimu wilayani Ngara walipokutana na Kupongezeana kwa Matokeo Mazuri ya Kidato cha Nne 2014. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, April 12, 2015

MAFANIKIO YA ELIMU:-Taswira Picha Wadau wa elimu wilayani Ngara walipokutana na Kupongezeana kwa Matokeo Mazuri ya Kidato cha Nne 2014.

Pichani ni  Katibu Tawala wa wilaya ya Ngara mkoani Kagera Bw.Vedastus Tibaijuka (Kushoto) na Afisa Elimu idara ya Sekondari wilaya Bw.Julius Nestory wakiwa pamoja wakati  Wadau wa Elimu wilayani Ngara ,mkoani Kagera walipokutana hivi karibuni katika ukumbi wa Shule ya sekondari Ngara mjini,pamoja na mambo mengine walijadili kuhusu ufaulu wa Kitaaluma na kupongezana baada ya shule kadha za Sekondari  kutoa matokeo bora ya Mtihani wa Kitaifa wa Kidaoto cha nne mwaka jana 2014,wilayani humo.


Miongoni mwa shule zilizofanya vizuri zaidi ni pamoja na Rulenge Sekondari,Rhec Sekondari, Shule ya Sekondari ya Wasichana Baramba  ambazo ni shule Binafsi wilayani humo pamoja na Shule ya sekondari Kanazi ambayo ni ya Serikali na kuifanya wilaya ya Ngara kushika nafasi ya 31 Kitaifa kati ya shule 16,693 za Sekondari nchini Tanzania.Habari/Picha na Shaban Ndyamukama.


Kushoto ni Meneja wa  Shule ya Sekondari ya Wasichana Baramba, Fr. Izias Bambara na mwenzake Meneja wa Rhec Sekondari, Bi.Helena Adrian wakilishana keki ya Kupongezana kwa Ushindi wa Matokeo mazuri ya shule zao ya Kidato cha Nne 2014.

Pichani ni  kushoto ni Muhitimu wa Kidato cha nne 2014 kutoka shule ya Sekondari Kirusha ,wilayani Ngara mkoani Kagera akitambulishwa na Mama yake Mazazi kulia mbele ya Wadau wa Elimu wilayani Ngara ,mkoani Kagera walipokutana hivi karibuni baada ya kuwa Mwanafunzi wa Kwanza kitaaluma katika mtihani huo na Idara ya Elimu Sekondari kuahidi kumlipia karo ya kidato cha tano na sita pamoja na nauli.

Kulia ni Mkuu wa Shule ya Sekondari Rhec,Bw.Venant akimkabisdhi cheti Mazazi wa Joshua,mhitimu aliyefanya vizuri katika Matokeo ya Kidato cha Nnne 2014.

Pata Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati  wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad