LIGI KUU BARA 2014/2015:-Azam FC sare ya pili leo April 11, 2015 huku Wagosi wakizinduka na ushindi wa 2 – 0. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, April 11, 2015

LIGI KUU BARA 2014/2015:-Azam FC sare ya pili leo April 11, 2015 huku Wagosi wakizinduka na ushindi wa 2 – 0.

Timu ya soka ya Azam FC sasa inahitaji miujiza kutetea Ubingwa wa Ligi kuu soka Tanzania bara msimu huu 2014/2015, baada ya kulazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na Mtibwa Sugar katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jioni ya leo April 11, 2015,kwenye Uwanja wa Manungu, Turiani, Morogoro.

Bao la Azam FC jioni ya leo limefungwa na kiungo Himid Mao Mkami, wakati la Mtibwa limefungwa na mshambuliaji mkongwe, Mussa Hassan Mgosi.

Matokeo hayo sasa yanaifanya Azam FC ifikishe pointi 38 baada ya kucheza mechi 20, sawa na vinara, Yanga SC wenye pointi 43.  

Sare hii ya pili mfululizo kwa Azam FC baada ya katikati ya wiki kutoka 1-1 pia na Mbeya City, rasmi inaanza kuitamanisha Simba SC kuwania nafasi ya pili.

Simba SC ina pointi 35 baada ya kucheza mechi 21 na itakutana na Azam FC wiki ijayo.

Kwenye mechi nyingine Leo April 11,2015,Coastal Union imeshinda mabao 2-0 dhidi ya JKT Ruvu Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.

Ikitoka kufungwa mabao 8-0 na Yanga SC, Coastal leo ilikuwa timu tofauti Chamazi, ikicheza soka maridadi na kupata ushindi muhimu wa ugenini.

Mabao ya Coastal yamefungwa na Rama Salim na Iker Obinna na sasa mabingwa hao wa Ligi Kuu 1988 wanafikisha pointi 27 baada ya kucheza mechi 23 na wanapanda hadi nafasi ya sita kutoka ya 11 kwenye msimamo wa ligi hiyo.

Siku ya Jumapili zipo Mechi mbili na Vinara wa Ligi Yanga wako Nyumbani Uwanja wa Taifa kucheza na Mbeya City ambayo iko Nafasi ya 7.

Jumapili Aprili 12,2015.

Yanga SC v Mbeya City

Stand United v Polisi Moro

LIGI KUU VODACOM MSIMAMO - 2014/2015.

1. Yanga SC Mechi 20 Pointi 43

2. Azam FC Mechi 20 Pointi 38

3. Simba SC Mechi 21 Pointi 35

Pata Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati  wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad