LA LIGA 2014/2015:-Picha FC Barcelona ikipata ugumu na gemu kuwa 2-2 sasa wawa Pointi 2 tu mbele ya Real Madrid. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, April 12, 2015

LA LIGA 2014/2015:-Picha FC Barcelona ikipata ugumu na gemu kuwa 2-2 sasa wawa Pointi 2 tu mbele ya Real Madrid.

Hapo jana April 11, 2015,usiku  huko Ugenini FC Barcelona walicheza na Sevilla ambayo haijafungwa kwao katika Mechi 31, na FC Barcelona  kukutana na ugumu wa kushinda mchezo  baada ya kutangulia kwa goli 2-0 na kujikuta wakitoka Sare 2-2 katika Mechi ya ligi kuu Hispania,La Liga.

 Matokeo hayo ya Sare  yanawafanya Barcelona waongoze La Liga kwa Pointi 2 tu mbele ya Real Madrid ambao Jana ilishinda 2-0 dhidi ya  2-0.


Katika mchezo huo  Barcelona walitangulia kwa Bao za Lionel Messi na Neymar za Dakika za 14 na 31 na Seville kurudisha katika Dakika za 38 na 84 kwa Bao za Ever Banega na Kevin Ganeiro.

Katika mchezo mwingine wa La Liga , timu ya  Malaga CF ilitoka sare ya 2-2 na  Atletico de Madrid huku Celta de Vigo ikishinda 6 – 1 dhidi ya  Rayo Vallecano na UD Almeria ikishinda 3 – 0 dhidi ya Granada CF.

Jumapili Aprili 12 ,2015.

1300 Getafe CF v Villarreal CF

1800 RCD Espanyol v Athletic de Bilba

2000 Real Sociedad v Deportivo La Coruna

2200 Cordoba CF v Elche CF

Jumatatu Aprili 13,2015.

2130 Valencia C.F v Levante


Pata Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati  wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad