Taratibu za
mahojiano zimekwishaanza kwa mujibu wa sheria na mtuhumiwa atapewa haki zote
anazostahili kama vile kuwa na ndugu yake wa karibu, rafiki yake anayemwamini
au wakili wake.
Kama ilivyo kawaida utakusanywa ushahidi kutoka pande zote za shauri hilo ili kubaini ukweli wa jinsi tukio hilo lilivyotokea na athari zake. Baada ya hapo hatua nyingine za kisheria zitachukuliwa ikiwa ni pamoja na kupata maoni ya kitaalamu na ya kisheria ili kuhakikisha kwamba haki inatendeka.
Ili ufanisi
upatikane katika upelelezi wa shauri hili, ni muhimu kupata ushirikiano kutoka
kwa kila atakayetakiwa kulisaidia Jeshi la Polisi kukamilisha haraka upelelezi wa
shauri hili ambalo sasa limepata mvuto mkubwa katika jamii.
Imetolewa na: S. H. KOVA KAMISHNA WA POLISI KANDA MAALUM DAR ES SALAAM
Pata
Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia
tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|
Katika hatua
nyingine…,’’Mara baada ya kuwasili katika kituo hicho alipokelewa kwa mahojiano
ya awali kutoka kwa vyombo vya habari ambapo Askofu Gwajima amesema maneno
aliyoyatoa ni ya kumkemea kiongozi mwenzake wa kiroho kwa madai ya kukiuka
msimamo wa viongozi wengine wa dini wa kuikataa mahakama ya kadhi.
Akijibu
swali kuhusu sababu za kufanya hivyo badala ya kutumia maneno ya kistaarabu ,Askofu
Gwajima amedai kuwa maneno aliyoyatoa ni maneno ya mungu huku akishangazwa na
wito wa Polisi kwa kuwa maneno hayo hakuyatoa kwa Jeshi la Polisi bali kwa kiongozi
mwenzie wa kiroho.
Askofu Gwajima alirekodiwa
kwenye ibada ya kanisa lake Jumapili iliyopita ambapo ‘alimtusi’ Pengo
akituhumu kuwa ni msaliti kwani amekwenda kinyume na Taasisi ya Baraza la
Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Baraza la Makanisa ya Kipentekoste (CPCT) na
Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) kwa kuwataka waumini waisome Katiba
Inayopendekezwa kisha wapewe uhuru wa kupiga kura ya “ndiyo” au “hapana”
tofauti na vyombo hivyo vyenye dhamana ya kuongoza dini ya Kikristo vilivyotaka
waumini waipigie kura ya “hapana” Katiba Inayopendekezwa.
No comments:
Post a Comment