Mpaka jana
March 05,2015, idadi ya watu waliopoteza maisha katika maafa hayo
yaliyosababishwa na mvua iliyonyesha ikiambatana mawe, upepo mkali na kubomoa
nyumba za wananchi Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga, ikiongezeka kutoka 42 na
kufikia 46, baadhi ya wananchi wa eneo hilo wamelihusisha janga hilo na
ushirikina.
Mwenyekiti
wa Serikali ya kijiji cha Mwakata wilayani Kahama, Salum Mohamed,alimweleza
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kuwa baadhi ya wananchi wamejenga dhana kuwa tukio
hilo limetokana na ushirikina.
Hata hivyo,
Pinda aliyewasili hapa jana, aliwataka wananchi hao kuachana na dhana hiyo
potofu kuwa mvua zilizonyesha na kusababisha maafa hayo, zimetokana na ushirikina.
Mvua hiyo
ilinyesha juzi March 03,2015 usiku na kuleta maafa katika vijiji vya Mwakata,
Nyumbi na Magung’hwa vilivyopo kata ya Isaka wilayani Kahama.
Idadi hiyo
imeongezeka kufuatia majeruhi wanne waliokuwa wamelazwa katika Hospitali ya
Wilaya ya Kahama kufariki dunia usiku wa kuamkia jana kuongeza idadi ya waliokufa katika janga hilo kufikia 46.BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
|
Mifugo nayo iliathiriwa na mvua hiyo kwa Kufa katika Kijiji cha
Mwakata,kata ya Isaka wilayani Kahama mkoani Shinyang’a baada ya mvua ya mawe iliyonyesha
kijijini hapo March 6, 2015.
|
UNGANA NASI KATIKA FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630. |
No comments:
Post a Comment