|
Katibu
Mtendaji wa NECTA, Dk. Charles Msonde.
Matokeo ya
mitihani ya kidato cha nne nchini ya mwaka 2014, yanatarajiwa kutangazwa na
Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA), Jumapili Februari 15,2015.
Katibu
Mtendaji wa Necta, Dk. Charles Msonde (pichani), alitoa ahadi hiyo kama zawadi
kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mpwapwa mkoani Dodoma, kufuatia ajali ya
moto iliyotokea Januari 20, mwaka huu na kuteketeza mali zote zilizokuwa
kwenye bweni la wasichana 64 wa kidato cha tano na cha sita.
Dk. Msonde
alikuwa miongoni mwa viongozi walioongozana na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri
Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi-Elimu), Kassim Majaliwa,
kwenye ziara ya kutoa pole katika shule hiyo.
“Zawadi
niliyowaandalia ni taarifa kwamba Februari 15, mwaka huu, tutatangaza matokeo
ya mitihani iliyofanywa na watahiniwa wa kidato cha nne nchini. Nasema ni
zawadi kwa sababu sijaitoa mahali kokote, nyie ndiyo wa kwanza kuipata,”
alieleza Msonde.
Watahiniwa
waliotarajiwa kufanya mtihani huo Novemba, mwaka jana 2014 ni 297,488 huku
watanihiwa 245,030 wakiwa wa shule na watahiniwa wa kujitegemea walikuwa
52,448. Watahiniwa wa shule walioandikishwa ni wavulana 132,244 (asilimia 53.97)
na wasichana 112,786 (asilimia 46.03).
Kwa kawaida,
matokeo ya kidato cha nne hutolewa Aprili, lakini mwaka huu yatatoka mapema
kutokana na uchaguzi mkuu wa Oktoba, mwaka huu. Walimu ni miongoni mwa
watumishi wa serikali ambao hutumiwa kusimamia uchaguzi mkuu.
Source:-Nipashe.
|
No comments:
Post a Comment