6. Philmon Charles.
Vijana walio
katika Wilaya ya Ngara waliahidiwa kupata ajira kupitia mradi wa Kabanga Nickel
na kwamba wazawa ndiyo wangepewa kipaumbele. Je, baada ya Kabanga Nickel
kutoanza uzalishaji na kutoa ajira amechukua hatua gani serikalini kujua sababu
za kukwama mradi huo na kuwaeleza wananchi sababu hizo?
Jibu: Nasikitika kwamba mradi wa Kabanga
Nickel ambao ulikuwa ni tegemeo kubwa la wananchi wa Ngara kwa kutoa ajira na
kusaidia huduma za jamii umesimama.
Umesimama kwa sababu bei ya Nickel kwenye
soko la dunia imeshuka sana kwa sababu China imeanzisha Nickel mbadala
inayopitiwa Nickel Pig Iron.
Serikali imenishirikisha sana katika sakata hili,
ikiwa ni pamoja na kunituma niende Canada mwaka jana kuzungumza na wawekezaji.
Hatimaye wawekezaji wa Canada wameamua kuuza hisa zao lakini hawajapata mnunuzi. Tuendelee kuwa na subira
huenda tukapata mwekezaji mwingine.
7. Askofu Dk Aaron Kijanjali.
Ahadi
zilikuwa nyingi ikiwa ni pamoja na kuondoa migogoro ya wakulima na wafugaji
kupitia mpango wa Mkurabita. Je, katika vijiji vya jimbo lako ni kipi
kimekwamisha wananchi wasitengewe maeneo kila kundi kujua sehemu ya matumizi
yake ya ardhi?
Jibu: Sikutoa ahadi ya kutatua migogoro ya
wakulima na wafugaji, lakini nimeshiriki bungeni katika kuiomba Serikali ambayo
inashughulikia tatizo hili la kitaifa.
Lakini nakiri kwamba ni mimi ambaye
nimeleta mpango wa Mkurabita Ngara kwa sababu naamini ni ukombozi kwa Mtanzania
wa kawaida.
Kupitia
mpango huo mashamba ya kaya yatapimwa na kupewa hati miliki ya kimila ambayo
inaweza ikatumika kama mdhamana na kupatia mikopo kutoka Benki.
Nakubaliana na
baba Askofu Kijanjari kwamba kwa kupitia utaratibu huu wa Mkurabita tunaweza
kumaliza mgogoro wa wakulima na wafugaji.
8. Hadija Hussen wa kata Bugarama-
Ngara.
Uliahidi
kijiji chetu cha Rwinyana kitapata maji kupitia Benki ya Dunia lakini hadi leo
hatuna maji hatuna zahanati wala kituo cha afya na wanawake tulio na bima za
afya ukienda Hospitali huudumiwi kama mwenye fedha tasilimu. Je, wewe unafanya
jitihada gani kutusaidia sisi wanawake?
Jibu: Mradi wa maji kwa kijiji cha
Rwinyana chini ya mradi wa maji wa Benki ya Dunia ulishaanza, lakini unasuasua
kwa sababu Serikali inatafuta fedha na imeahidi kumaliza tatizo la maji kwa
kijiji hicho kabla ya Juni mwaka huu.
Bima ya Afya ni muhimu sana kwa mwananchi
yeyote. Tatizo la watoa huduma wakorofi ni la muda, tatizo kubwa lililopo ni
upungufu wa dawa ambalo linashughulikiwa na Serikali.
Wananchi wa Rwinyana sasa
hivi wanatumia Kituo cha Afya Bukiriro na Sera ya Serikali ni kuwa na kituo cha
afya kila kata na zahanati kila kijiji. Naamini fedha za Serikali ikiboreka
kata ya Bugarama inapata kituo cha afya.
9. Martin Mwampamba mkazi wa Rulenge.
Wakati ukiomba kura kwa wananchi ulisema mara vikao
vikiisha utakuja kuishi jimboni siyo Dar es Salaam. Je? Mbona hadi unamaliza
kipindi chako cha uongozi hukai jimboni na kufanya mikutano ya hadhara na
wananchi kusikiliza kero zao? Ahadi hiyo imekuaje ukashindwa kuitekeleza?
Jibu: Ndugu Martin Mwampamba unajua fika
kwamba huwa nakuja Rulenge nyumbani kwangu na huwa nahudhuria mikutano ya
kijiji cha Rulenge na kufanya mikutano ya hadhara lakini ukumbuke kwamba
ninapokuwa Dar es Salaam nakutana na watendaji wa wizara pamoja na mashirika
kama REA na kujadili masuala ya umeme.
Mara nyingi natembea wizara ya maji
kuwaomba watoe fedha kwa ajili ya maji ndiyo maana tumeweza kupata umeme wa
Rulenge na maji kwa ajili ya vijiji vya Rulenge na Munjebwe.
Huwa nagawa muda
wangu kati ya Ngara na Dar es Salaam ‘Akanyoni katugurutse ntikamenya iyo
bweze’ nikikaa Rulenge muda wote haisaidii kimarendeleo.
10. Seth Feruzi mkazi wa Ngara Mjini.
Uliahidi
vijana wa mijini na vijijini kuwaunganisha na kuwapatia vifaa vya michezo ili
washiriki kwenye timu mbalimbali na kucheza ligi hadi ngazi ya Taifa cha
kushangaza hakuna timu uliyoipatia vifaa vya michezo wala kuanzisha ligi ya
mbunge. Je, ahadi hiyo unategemea kuitekeleza lini kwa wananchi wa jimbo lako?
Jibu:
Sikutoa ahadi ya kutoa vifaa vya michezo kwa vijana wa mijini na vijijini. Hata
hivyo nimetoa jezi na mipira kwa baadhi ya vijiji nitaendelea kufanya hivyo kwa
kipindi kidogo kilichobaki.
Source:-Mwananchi.
|
Friday, February 27, 2015
MASWALI / MAJIBU :-10 Kwa Mbunge wangu, Deogratias Ntukamazina
Tags
# SIASA
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
SIASA
Labels:
SIASA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment